Hospitali
ya Taifa Muhimbili (MNH) imepata mafanikio makubwa baada ya kufanya
upasuaji wa kupandikiza vifaa vya kusaidia kusikia kwa watoto 21 ndani
ya miezi 17 ukilinganisha na watoto 50 waliopandikizwa vifaa hivyo miaka
15 iliyopita nchini India.
Kila mwaka Serikali ilikuwa ikipeleka wagonjwa nchini India kwa ajili ya kupandikizwa vya vifaa vya kusaidia kusikia na hadi kufikia mwaka 2016, wagonjwa 50 tu walikuwa wamenufaika na huduma hiyo.
Akizungumza na waandishi wa habari leo, Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Masikio, Pua na Koo wa Muhimbili, Dkt. Edwin Liyombo amefafanua kwamba hospitali hiyo itavunja rekodi kwa kuwa hadi sasa tayari wagonjwa 21 ndani ya miezi 17 kuanzia Juni mwaka 2017 hadi Novemba 2018 sawa na asilimia 42 wamepatiwa matibabu tofauti na wagonjwa 50 waliopelekwa India katika kipindi cha miaka 15 iliyopita kuanzia 2003 hadi 2016.
Dkt. Liyombo amesema mwaka 2003 Serikali ilianza kupeleka wagonjwa nchini India kwa ajili ya kupandikizwa vifaa vya kusadia kusikia na kwamba idadi ya wagonjwa imekuwa ikiongezeka. Dkt. Liyombo amesema kwamba gharama ya kutoa huduma hiyo kwa mgonjwa mmoja katika Hospotali ya Taifa Muhimbili ni Tshs. 37 milioni wakati India kwa mgonjwa mmoja ni Tshs. 80 milioni hadi Tshs. 100 milioni.
Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Masikio, Pua na Koo wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Dkt. Edwin Liyombo akizungumza na waandishi wa habari kuhusu upasuaji wa kupandikiza vifaa vya kusaidia kusikia kwa watoto 10 ambao umefanywa na wataalam wa Muhimbili kwa kushirikiana na mtaalam kutoka nchini Misri.
Watoto waliopandikizwa vifaa vya kusaidia kusikia wakiwa wodini baada ya kupatiwa huduma hiyo.
Pichani ni baadhi ya watoto waliopandikizwa vifaa hivyo.

Dkt. Liyombo akiwaeleza waandishi wa habari jinsi vifaa vya kusaidia kusikia vinavyofanya kazi baada ya mwezi mmoja.
Kila mwaka Serikali ilikuwa ikipeleka wagonjwa nchini India kwa ajili ya kupandikizwa vya vifaa vya kusaidia kusikia na hadi kufikia mwaka 2016, wagonjwa 50 tu walikuwa wamenufaika na huduma hiyo.
Akizungumza na waandishi wa habari leo, Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Masikio, Pua na Koo wa Muhimbili, Dkt. Edwin Liyombo amefafanua kwamba hospitali hiyo itavunja rekodi kwa kuwa hadi sasa tayari wagonjwa 21 ndani ya miezi 17 kuanzia Juni mwaka 2017 hadi Novemba 2018 sawa na asilimia 42 wamepatiwa matibabu tofauti na wagonjwa 50 waliopelekwa India katika kipindi cha miaka 15 iliyopita kuanzia 2003 hadi 2016.
Dkt. Liyombo amesema mwaka 2003 Serikali ilianza kupeleka wagonjwa nchini India kwa ajili ya kupandikizwa vifaa vya kusadia kusikia na kwamba idadi ya wagonjwa imekuwa ikiongezeka. Dkt. Liyombo amesema kwamba gharama ya kutoa huduma hiyo kwa mgonjwa mmoja katika Hospotali ya Taifa Muhimbili ni Tshs. 37 milioni wakati India kwa mgonjwa mmoja ni Tshs. 80 milioni hadi Tshs. 100 milioni.

Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Masikio, Pua na Koo wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Dkt. Edwin Liyombo akizungumza na waandishi wa habari kuhusu upasuaji wa kupandikiza vifaa vya kusaidia kusikia kwa watoto 10 ambao umefanywa na wataalam wa Muhimbili kwa kushirikiana na mtaalam kutoka nchini Misri.
Watoto waliopandikizwa vifaa vya kusaidia kusikia wakiwa wodini baada ya kupatiwa huduma hiyo.
Pichani ni baadhi ya watoto waliopandikizwa vifaa hivyo.
Dkt. Liyombo akiwaeleza waandishi wa habari jinsi vifaa vya kusaidia kusikia vinavyofanya kazi baada ya mwezi mmoja.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...