Na Mathias Canal-NFRA, Dodoma

Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Innocent Bashungwa amefanya ziara ya kikazi kwa kutembelea na kujionea shughuli zinazofanywa na Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) Jijini Dodoma.

Katika ziara hiyo Mhe Bashungwa amekagua ujenzi wa Maghala na Vihenge vya Kisasa (Silos) ambapo ameipongeza serikali ya awamu ya Tano inayoongozwa na Mhe Rais Dkt John Pombe Magufuli kwa kuanzisha ujenzi wa mradi huo utakaoongeza uwezo wa kuhifadhi nafaka.

Akizungumza na wafanyakazi wa NFRA mara baada ya kuzuru katika ofisi hizo zilizopo Mtaa wa Relini-Kizota Mhe Bashungwa alisema kuwa uongozi imara wa Dkt Magufuli umepelekea Serikali ya Tanzania na Serikali ya Poland kusaini mkataba wa mkopo wa masharti nafuu Septemba 2015 wa Dola milioni 55 sawa na sh. bilioni 124, kwa ajili ya ujenzi wa mradi huo, ambao utaongeza uwezo wa hifadhi ya chakula.

Katika hatua nyingine Naibu Waziri huyo ametoa rai kwa Mtendaji Mkuu wa wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula NFRA Bi Vumilia L. Zikankuba kuweka msisitizo zaidi katika utoaji elimu kwa wakulima kuhusu njia bora za kuhifadhi mahindi ili wakati wanapotafuta soko waweze kupata soko imara na tija kutokana na nafaka hiyo.

Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Innocent Bashungwa 
Mtendaji Mkuu wa wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula NFRA Bi Vumilia L. Zikankuba


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...