NA MWANDISHI WETU
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera na Uratibu Prof.Faustin Kamuzora amewataka wakulima wa Wilaya ya Kasulu kulima kwa tija ili kuondokana na changamoto wanazokabiliana nazo ikiwa ni pamoja na ukosefu wa masoko.

Ametoa kauli hiyo Novemba 08, 2018 alipofanya ziara katika maeneo ya Mradi wa Kuboresha Mazingira ya Biashara Local Investment Climate (LIC) ikiwemo Mradi wa Umwagiliaji wa Tittye Wilayani Kasulu mkoani Kigoma ili kukagua na kujiridhisha ubora na faida zitokanazo na mradi huo.

“Wakulima wa Wilaya ya Kasulu hamna budi kubadili mitazamo katika uzalishaji kwa kuanza kuweka mikakati ya kuzalisha kwa tija ili kuondokana na changamoto za kukosa masoko ya mazao ikiwemo Mpunga na mihogo hivyo ni wakati muafaka kuwatumia maafisa kilimo waliopo ili kupata mbinu mbadala za matumizi mazuri ya pembejeo za kisasa ili kuzalisha kwa tija”.Alisema Prof.Kamuzora

Aliongezea kuwa wakulima wanapaswa kuondokana na dhana potofu ya kilimo cha asili kinachohusisha dhana ya kulima kwa dawa za kienyeji ambazo wamekuwa wakizitumia kwa muda mrefu bila kuleta matunda wanayotarajiwa.

“Ni vyema sasa kuachana na kilimo cha matumizi ya dawa za kienyeji na hatimaye muone namna bora ya kuwatumia wataalam wa masuala ya kilimo ili  kuendana na mabadiliko ya sayansi na teknolojia ili kuzalisha kwa tija.”Alisisitiza Prof.Kamuzora

Naye Mkuu wa Wilaya ya Kasulu Mhe.Kanali Simon Anange aliahidi kutekeleza maagizo yaliyotolewa na Katibu Mkuu huyo pamoja na kutoa rai kwa wakulima wa Kasulu kuendelea kuzalisha kwa tija ili kuendana na soko lililopo.
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu) Prof.Faustin Kamuzora (wa kwanza kushoto) akiuliza jambo kwa Mkurugenzi wa Kasulu Vijijini Mhandisi Godfrey Kasekenya alipotembelea kukagua mradi wa Umwagiliaji wa mashamba ya mpunga wa Titye uliojengwa na Mradi wa Kuboresha Mazingira ya Biashara (Local Investment Climate -LIC) unaoratibiwa na Baraza la Taifa la Biashara (TNBC) uliopo Wilaya ya Kasulu mkoani Kigoama Novemba 08, 2018.
Mkuu wa Wilaya ya Kasulu Mhe.Kanali Simon Anange akizungumza jambo wakati wa kikao cha pamoja na Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu) Prof.Faustin Kamuzora alipotembelea ofisini kwake kwa lengo la kupata taarifa za miradi inayotekelezwa chini ya uratibu wa Baraza la Taifa la Biashara (TNBC).
Kaimu Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Biashara Bi.Oliver Ligula akichangia jambo wakati wa kikao na Mkuu wa Wilaya ya Kasulu Mhe.Kanali Simon Anange pamoja na baadhi ya Watendaji wa Wilaya hiyo walipotembelea kukagua utekelezaji wa Mradi wa Kuboresha Mazingira ya Biashara ( Local Investment Climate -LIC) katika Wilaya hiyo.
Afisa wa Baraza la Biashara la Taifa na Mratibu wa shughuli za Mabaraza ya Biashara Kigoma Bw. Ano Mwamsiku akieleza mafanikio ya mabaraza ya biashara kwa Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Prof.Faustin Kamuzora (hayupo pichani) wakati wa kikao cha pamoja na Watendaji wa Wilaya ya Kasulu walipotembelea kupata taarifa za utekelezaji wa miradi ya LIC.
Baadhi ya wajumbe wa kikao cha kupokea taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Umwagiliaji ya mashamba ya mpunga ya Titye inayofadhiliwa na Mradi wa Kuboresha Mazingira ya Biashara (Local Investment Climate -LIC) Wilayani Kasulu Mkoani  Kigoma.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...