*Aeleza namna Serikali inavyotekeleza miradi bila wafadhili
Na Said Mwishehe,Globu ya jamii
RAIS Dk.John Magufuli amewahakikishia Watanzania kuwa hivi sasa Serikali yake inayo fedha za kutosha ambayo inaweza kuiendesha nchi kwa miezi sita kwa kununua bidhaa bila tatizo lolote huku akieleza kuwa fedha zilizopo ndio maana wakati mwingine zinasababisha kiburi
ambacho wakubwa hawapendi.
Dk.Magufuli amesema hayo leo kwenye Kongamano la uchumi lililofanyika katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambapo pamoja na kuelezea mambo mbalimbali ambayo yamefanywa na Serikali ya Awamu ya Tano amezungumzia namna ambavyo wamefanikiwa kudhibiti upotevu wa fedha.
"Tuna pesa za kufanya mambo yetu na unapokuwa na pesa wakati mwingine unakuwa na jeuri ambayo hata hivyo haipendwi na wakubwa.Ukweli ni kwamba tumeziba mirija ya kuvujisha fedha na ndio maana hata makusanyo yameongezeka,"amesema.Amefafanua katika jitihada za kuziba upotevu wa fedha Serikali yake iliamua kuweka mkakati wa kuondoa watumishi hewa ambapo kwa mwezi Serikali ilikuwa inalipa Sh.bilioni 423 kwa mwaka kwa watu ambao hawapo."Kwa mwezi tulikuwa tunalipa mshahara wa Sh.bilioni 777 na bada ya uhakiki mishara inayolipwa kwa mwezi ni Sh.bilioni 251 kwa mwezi,"amesema Rais Magufuli.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...