Dar es Salaam: Novemba 5, 2018, Kaimu Balozi wa Marekani nchini Tanzania Dkt. Inmi
Patterson na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais wa Muungano na Mazingira Ndugu
January Makamba wamezindua mradi utakaogharimu kiasi cha dola za kimarekani milioni 20 ili
kuboresha usimamizi katika kuhifadhi mazingira kwenye ukanda wa magharibi mwa Tanzania.
Mradi huu wa uhifadhi wa mazingira unafadhiliwa na Serikali ya Marekani kupitia Shirika lake
la Maendeleo ya Kimataifa (USAID) na utatekelezwa kwa ushirikiano wa pamoja na Taasisi ya
Jane Goodall (JGI).
Mradi huu mpya utasaidia watu wa Mikoa ya Kigoma na Katavi, pamoja na serikali za mitaa,
katika utekelezaji wa mipango ya matumizi bora ya ardhi na utakaonufaisha vijiji 104.
Mradi huu wa Uhifadhi wa Mazingira umeundwa kulinda mazingira wakati pia unasaidia
wananchi katika shuhuli za kujikimu kiuchumi na maisha bora kama vile uzalishaji wa kahawa
na utalii asili kwa ajili ya watanzania. Taasisi ya Jane Goodall itafanya kazi kwa karibu na jamii
ili kuhamasisha mazoea endelevu zaidi ya usimamizi wa ardhi na kukuza elimu ya mazingira,
kwa kutumia majukwaa kama vile mradi iliyofanikiwa sana ya Roots na Shoots ya Taasisi ya
Jane Goodall.
Zaidi ya hayo, kama sehemu ya ruzuku hii, Taasisi ya Jane Goodall itaendelea kufanya kazi kwa
kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika kuunda mifumo imara zaidi katika kuhifadhi na
kulinda sokwe walioko ndani na nje ya maeneo tengefu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...