Na Ripota Wetu,Globu ya jamii
SHIRIKA
la Kimataifa la Hifadhi la World Wide Fund for Nature (WWF) limefanya
ziara katika Wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma kwa lengo la kufuatilia
maendeleo ya utekelezaji wa mradi ujulikanao SECAD program ( Selous
Eco-system Conservation and Development program).
SECAD
ni mradi ambao kwa jumla utatekelezwa kwa miaka mitano ikiwa ni awamu
ya kwanza na ya pili ambapo umejikita kuhakikisha wanaongeza uhifadhi wa
mazingira kwa maana ya kwenye hifadhi ya Selous pamoja na ushoroba
(corridor) unaounganisha pori la akiba la Selous na hifadhi ya Niassa
ipatikanayo nchini Msumbiji
Mkuu
wa Wilaya Namtumbo Sophia Kizigo jana kwamba ugeni wa shirika hili
uliofika wilayani kwake ulitembelea na kujionea maendeleo ya mradi na
kutembelea jumuiya ya uhifadhi ya Mbarang'andu ambapo walipata taarifa
ya mradi na kujionea mafanikio, mipango na changamoto kwa sasa.
Mkuu
wa Wilaya huyo ameueleza ugeni wa shirika hilo kuwa moja ya mafanikio
ni mradi wa ufugaji wa nyuki kwa ajili ya kurina asali ambao
unaosimamiwa na jumuiya hiyo pamoja na mpango wa ujenzi wa kiwanda cha
kuongezea thamani asali pamoja na mabwawa ya samaki.
Kuhusu
changamoto amesema moja ya changamoto ya mradi ni wananchi kuvamia
maeneo ya hifadhi na kufanya shughuli za kibinadamu kama kilimo na
ufugaji
Pia walitembelea Chuo cha Likuyu ambacho kinatumika kufundisha VGS (village scouts) wanaotumika kulinda hifadhi hizo.
Mkuu wa Wilaya Namtumbo Sophia Kizigo akipewa maelezo kuhusiana na maendeleo ya mradi wa wa SECAD program ( Selous Eco-system Conservation and Development program) wakati SHIRIKA la Kimataifa la Hifadhi la World Wide Fund for Nature (WWF) likifanya zaira wilayani yumo kufuatilia mradi huo
Eneo la mradi wa ufugaji wa nyuki kwa ajili ya kurina asali
Mkuu wa Wilaya Namtumbo Sophia Kizigo akiwa sambamba na Wadau wa SHIRIKA la Kimataifa la Hifadhi la World Wide Fund for Nature (WWF) wakionesha chupa ya asali ikiwa ni sehemu ya mafanikio
ya mradi wa ufugaji wa nyuki kwa ajili ya kurina asali ,ambao
unasimamiwa na jumuiya hiyo pamoja na mpango wa ujenzi wa kiwanda cha
kuongezea thamani asali pamoja na mabwawa ya samaki.
Mkuu wa Wilaya Namtumbo Sophia Kizigo akikaribishwa mara baada ya kuwapokea wageni kutoka SHIRIKA
la Kimataifa la Hifadhi la World Wide Fund for Nature (WWF) llilofanya
ziara katika Wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma kwa lengo la kufuatilia
maendeleo ya utekelezaji wa mradi ujulikanao SECAD program ( Selous
Eco-system Conservation and Development program).
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...