-Baadhi ya Wabunge wapanda jukwaani kusakata Kwaito, Bolingo
-Bill Nas, Weusi , Whozu, Rosaree waacha historia


Wabunge na viongozi wa Serikali, jana walikuwa ni sehemu ya burudani ya aina yake katika Tamasha kubwa la muziki la Tigo Fiesta 2018, lililofanyika katika uwanja wa Jamuhuri mjini Dodoma.

Tamasha hilo lililofanikiwa kuwavuta mashabiki wa muziki wa bongo fleva kutoka mkoa huo na viunga vyake, lilianza kwa msanii Jay Melody kupanda jukwaani na kutoa burudani safi ‘iliyobamba’na kutengeneza mazingira safi kwa waliomfuatia .

Baada ya wasanii kadhaa kupanda jukwaani i, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Patrobas Katambi alipanda jukwaani kuongea mawili matatu kabla ya kuomba kuwekewa muziki wa bolingo ambalo alisakata kwa ustadi kmubwa jambo lililozua shangwe za ktosha.

Wakati Katambi akiendelea kusakata bolingo, baadhi ya wabunge wakiongozwa na mbunge wa Sengerema William Ngeleja waliomba kuwekewa muziki wa Kwaito ambao waliusakata kwa ufundi mkubwa na kusababisha shangwe kubwa kutoka kwa mashabiki.
 Baadhi ya Wabunge na viongozi wa Serikali wakisakata muziki katika Tamasha la Tigo Fiesta mwaka 2018 lililofanyika katika uwanja wa Jamuhuri Mkoani Dodoma mwishoni mwa wiki.
 Msanii wa muziki wa Hip Hop Fid Q akiwapagawisha mamia ya mashabiki walioshiriki katika tamasha la Tigo Fiesta mwaka 2018 lililofanyika uwanja wa Jamuhuri mkoani Dodoma.
 Msanii anayefanya vizuri kwenye muziki wa Hip Hop Rich Mavoko,  akiwaburudisha  mamia ya wakazi wa mkoa wa Dodoma na maeneo jirani walioshiriki katika Tamasha la Tigo Fiesta mwaka 2018 lililofanyika katika uwanja wa Jamuhuri Mkoani humo. 

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>>>

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...