Waziri wa Madini, Angellah Kairuki (kulia) akizungumza wakati makabidhiano ya mashine ya kusaidia kupumua kwa Watoto njiti ilivyotolewa na taasisi ya Vodacom Tanzania Foundation kwa hospitali ya rufaa ya mkoa wa Dodoma ili kusaidia kupunguza vifo vya Watoto Njiti. Kushoto ni Mkurugenzi wa Vodacom Tanzania Foundation Rosalynn Mworia, Mkurugenzi wa Taasisi ya Doris Mollel, Doris Mollel (kati).

Mkurugenzi wa Vodacom Tanzania Foundation Rosalynn Mworia, akikabidhi mashine ya kusaidia kupumua kwa Watoto njiti kwa Waziri wa Madini Angellah Kairuki (wa pili kulia) na Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayesimamia Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na walemavu Anthony Mavunde (kulia) katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Dodoma ili kusaidia kupunguza vifo vya Watoto Njiti. Wa pili kushoto ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Doris Mollel, Bi Doris Mollel.
Afisa Muuguzi Msaidizi kutoka Kitengo cha kuhudumia Watoto Njiti Constancia Mankupe akielezea kwa vitendo namna mashine ya kusaidia kupumua kwa Watoto njiti inavyofanya kazi, mashine hii ni mojawapo kati ya vifaa tiba vyenye thamani Sh 25 m vilivyotolewa na taasisi ya Vodacom Tanzania Foundation vilivyokabidhiwa kwa hospitali ya rufaa ya mkoa wa Dodoma ili kusaidia kupunguza vifo vya Watoto Njiti. Kulia kwake ni Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayesimamia Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na walemavu Anthony Mavunde na Mkurugenzi wa Taasisi ya Doris Mollel, Doris Mollel.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...