*Naibu Gavana ahimiza uwajibikaji kwa waandishi wa habari nchini
Na Said Mwishehe,Globu ya jamii
BENKI Kuu ya Tanzania(BoT) ,imesema imeamua kuanzisha utaratibu wa kuendesha semina kwa waandishi wa habari wa vyombo vya habari nchini kwa lengo la kukuza uandishi wa habari za uchumi na fedha.
Pia lengo la semina hiyo kwa waandishi wa habari nchini ni kuelimisha na kufafanua masuala yanayohusu majukumu na kazi za Benki Kuu , kujenga uwezo wa kutafsiri na kuchambua taarifa za uchumi na fedha, kuboresha na kudumisha uhusiano mzuri wa kikazoi kati ya vyombo vya habari na BoT.
Malengo mengine ya semina hiyo ni kupata mrejesho kutoka kwa waandishi wa habari kuhusu utendaji wao wa kazi na njia bora ya kudumisha mawasiliano baina ya taasisi zao.
Na Said Mwishehe,Globu ya jamii
BENKI Kuu ya Tanzania(BoT) ,imesema imeamua kuanzisha utaratibu wa kuendesha semina kwa waandishi wa habari wa vyombo vya habari nchini kwa lengo la kukuza uandishi wa habari za uchumi na fedha.
Pia lengo la semina hiyo kwa waandishi wa habari nchini ni kuelimisha na kufafanua masuala yanayohusu majukumu na kazi za Benki Kuu , kujenga uwezo wa kutafsiri na kuchambua taarifa za uchumi na fedha, kuboresha na kudumisha uhusiano mzuri wa kikazoi kati ya vyombo vya habari na BoT.
Malengo mengine ya semina hiyo ni kupata mrejesho kutoka kwa waandishi wa habari kuhusu utendaji wao wa kazi na njia bora ya kudumisha mawasiliano baina ya taasisi zao.
Hotuba
ya Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) upande wa Uchumi na Sera
Dk. Yamungu Kayandabila ambayo imesomwa kwa niaba yake na Mkurugenzi wa
Tawi la Benki Kuu Dodoma Richard Wambali amesema benki hiyo inatambua
mchango wa vyombo vya habari nchini katika kuufahamisha umma wa
Watazanzania na dunia
kwa ujumla.
"Mara kadhaa mmekuwa msaada mkubwa sana katika kutufikishia taarifa zetu kwa umma, na wakati mwingine baada ya kupokea mwito wa muda mfupi.Pia kupitia kazi zenu mnatuwezesha kujua ni nini wananchi wanasema au kutarajia kutoka katika taasisi zetu."Benki Kuu ya Tanzania imekuwa ikiendesha semina kama hii, tumeshuhudia kuimarika kwa uandishi wa habari za uchumi na fedha katika vyombo mbalimbali vya habari.Matokeo haya mema yametupa uthibitisho kwamba mafunzo tunayotoa kwa wadau wetu wakuu yana manufaa makubwa,"amesema.
kwa ujumla.
"Mara kadhaa mmekuwa msaada mkubwa sana katika kutufikishia taarifa zetu kwa umma, na wakati mwingine baada ya kupokea mwito wa muda mfupi.Pia kupitia kazi zenu mnatuwezesha kujua ni nini wananchi wanasema au kutarajia kutoka katika taasisi zetu."Benki Kuu ya Tanzania imekuwa ikiendesha semina kama hii, tumeshuhudia kuimarika kwa uandishi wa habari za uchumi na fedha katika vyombo mbalimbali vya habari.Matokeo haya mema yametupa uthibitisho kwamba mafunzo tunayotoa kwa wadau wetu wakuu yana manufaa makubwa,"amesema.
Mkurugenzi
wa Benki Kuu ya Tanzania tawi la Dodoma Bw. Richard Wambali
aliyemwakilisha Dkt. Yamungu Kayandabila Naibu Gavana anayeshughulikia
Uchumi na Fedha akifungua semina ya siku tano ya waandishi wa habari
kutoka vyombo mbalimbali kuhusu masuala ya uchumi na fedha inayofanyika
kwenye ukumbi wa (BOT) jijini Dodoma.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...