Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe Jerry Muro amezindua kampeni ya kuhamasisha utalii wa Ndani Kwa kuwataka wananchi kutenga muda wa kutembelea vivutio vya utalii vilivyopo nchini .
Mhe Muro amewataka Watanzania wanaotoka katika mikoa ya kanda ya Kaskazini Tanga,Kilimanjaro, Arusha na Manyara ambao Wana tabia ya kwenda nyumbani nyakati za sikukuu ya Xmass na Mwaka mpya kuweka utamaduni wa kutembelea pia Hifadhi za taifa za Wanyama zilizojirani na maeneo yao ikiwemo Hifadhi pekee ya taifa ya Arusha ambayo iko mjini Kabisa .
Mhe Muro amewapongeza Wafanyakazi na Mhifadhi Mkuu wa Arusha National Parks Kwa uamuzi wao wa kuhamasisha utalii wa ndani Kwa kupunguza Ada ya viingilio pamoja na kufanya maandalizi ya kutoa Usafiri maalum utakaobeba wananchi na kuwapeleka kwenye hifadhi ili kutoa nafasi Kwa wananchi wengi zaidi kutembelea hifadhi ya Wanyama Arusha
Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe Jerry Muro akizindua kampeni ya kuhamasisha utalii wa Ndani kwa kuwataka wananchi kutenga muda wa kutembelea vivutio vya utalii vilivyopo nchini
Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe Jerry Muro akizungumza na baadhi ya Wananchi wakati wa hafla ya uzinduzi wa kampeni ya kuhamasisha utalii wa Ndani kwa kuwataka wananchi kutenga muda wa kutembelea vivutio vya utalii vilivyopo nchini
Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe Jerry Muro akiwa na furaha tele baada ya kuzindua kampeni ya kuhamasisha utalii wa Ndani kwa kuwataka wananchi kutenga muda wa kutembelea vivutio vya utalii vilivyopo nchini.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...