SERIKALI ya Awamu ya Tano imeendelea kutumia ubunifu katika kuwahudumia wananchi ikiwemo kujibu na kufafanua kero zao papo kwa papo.

Katika hatua isiyokuwa ya kawaida, Msemaji Mkuu wa Serikali leo akiwa ziarani mkoani Morogoro alilazimika kuwapigia simu baadhi ya watendaji wa Serikali akiwa moja kwa moja studio za Redio Abood FM na ATV ili wajibu kero za sekta zao.

Afisa wa kwanza kukumbana na "kibano" hicho alikuwa Meneja Mawasiliano wa Mamlaka ya Hifadhi za Taifa (TANAPA), Bw. Paschal Shelutete ambaye alipigiwa kwa mstukizo na kuunganishwa moja kwa moja studio ili ajibu swali la mwananchi aliyelalamikia tembo kutoka hifadhi mbalimbali kuvamia mashamba ya wananchi na kuharibu mazao.

Bw. Shelutete akionekana kulijua vyema eneo lake alifafanua kuwa kutokana na changamoto hiyo Tanapa na Mamlaka nyingine za Serikali kama Idara ya Wanyamapori zimekuwa na programu za kuwaelimisha wananchi wanaokaa karibu na hifadhi na mapori ya akiba.

"Tunaendelea kuwaelimisha wananchi wahakikishe wanatoa taarifa hizi kila wanapowaona wanyama wa porini wanarandaranda katika maeneo yao ili mamlaka zichukue hatua stahiki," alifafanua akitoa maelekezo ya hatua za kufuatwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...