Jumia imewakabidhi wakazi wa jijini Dar es Salaam, Bw. Johnson Kiama na Dismas Kamalamo zawadi za pikipiki na luninga mpya ya kisasa walizojishindia kupitia shindano la ‘Treasure Hunt.’

Shindano hilo lilikuwa likifanyika kila siku ya Ijumaa kupitia kampeni kubwa ya mauzo ya mwaka ya Jumia inayokwenda kwa Black Friday. Kampeni hiyo ambayo ilianza Novemba 16 na kufikia ukomo Ijumaa iliyopita ya Desemba 7, imewawezesha wateja kufanya manunuzi yao ya msimu huu wa sikukuu kwa ofa na punguzo kubwa la bei mpaka 70%!

Zawadi zote mbili za pikipiki na luninga zilifichwa kwenye mtandao wa Jumia ambapo wateja walitakiwa kuzisaka na kukabidhiwa kwa punguzo la asilimia 99 mara baada ya kuzipata. Zoezi hilo lilifanyika kupitia njia ya App ya Jumia inayopatikana kwenye simu zote za iPhone (Apple Store) na Android (Google Play Store). Dhumuni lilikuwa ni kuwawezesha wateja wengi zaidi, ambao wanamiliki simu za kisasa za mkononi, kushiriki mahali popote na muda wowote walipo.

Pikipiki hiyo aliyokabidhiwa mshindi, aina ya Skymark, inauzwa kwa shilingi 1,850,000 katika mtandao wa Jumia. Lakini mshindi amekabidhiwa kwa kulipia shilingi 18,500 tu ambayo ni sawa na punguzo la asilimia 99!Huku naye mshindi wa luninga mpya na ya kisasa aina ya Bruhm yenye ukubwa wa inchi 32 yenyewe inauzwa kwa shilingi 570,000 kwenye mtandao wa Jumia. Lakini mshindi amekabidhiwa kwa kulipia shilingi 5,700 tu ambayo ni sawa na punguzo la asilimia 99!

Akielezea namna atakavyoitumia zawadi yake ya pikipiki mara baada ya kukabidhiwa, Bw. Johnson Kiama, amesema kuwa, “siamini kama leo hii nimekabidhiwa hii pikipiki maana ilinichukua muda mrefu kuipata. 
  Meneja Mahusiano ya Umma wa Jumia Tanzania, Kijanga Geofrey akizungumza mbele ya Waandishi wa Habari jijini Dar leo wakati wakikabidhi  wakazi wawili wa jijini Dar es Salaam, Bw. Johnson Kiama na Dismas Kamalamo zawadi za pikipiki na luninga mpya ya kisasa walizojishindia kupitia shindano la ‘Treasure Hunt.’
 Meneja Mahusiano ya Umma wa Jumia Tanzania, Kijanga Geofrey akimkabidhi  mbele ya Waandishi wa habari,Bw. Johnson Kiama luninga mpya ya kisasa aliyojishindia kupitia shindano la ‘Treasure Hunt.’
Meneja Mahusiano ya Umma wa Jumia Tanzania, Kijanga Geofrey akimkabidhi  ufunguo wa piki piki Dismas Kamalamo mbele ya Waandishi wa habari, aliyojishindia kupitia shindano la ‘Treasure Hunt.’

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...