“Hata ingawa ninatembea katika bonde lenye kivuli kizito, Siogopi chochote kibaya,Kwa maana wewe uko pamoja nami; Fimbo yako na gongo lako ndivyo vitu vinavyonifariji.” (Zaburi 23:4)

LUTENI KANALI (MSTAAFU) WILLY JOHN MASOI

Miaka 4 imetimia leo tangu Mwenyezi Mungu alipokuita kwake. Hata hivyo kutokana na upendo wako kwetu tunaamini Baba yetu kipenzi unaendelea kutulinda, kutusimamia na kutuongoza katika kila tufanyalo. Baba, endelea kuimba na Malaika.

Unakumbukwa na mke wako kipenzi Mary-Salome, watoto, wakwe, wajukuu, shemeji, ndugu, jamaa, marafiki na majirani zako.

Raha ya Milele umpe, ee Bwana, na Mwanga wa Milele Uingazie Roho ya Marehemu Luteni Kanali (Mstaafu) Willy John Masoi. Apumzike kwa Amani, Amina. Zab: 23:4

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...