Na Munir Shemweta, WANMM
Waziri wa ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi amesema halmashauri zina wajibu wa kuayasimamia mabaraza ya ardhi ya Kata katika maeneo mablimbali nchini.

Kauli ya Lukuvi inafuatia Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda kumeleza kuwa ofisi yake hairidhishwi na namna  Mabaraza ya Ardhi ya Kata yanayofanya kazi  na kubainisha kuwa baadhi yake yanaendeshwa na watu wasiokuwa na taluma ya sheria huku wakitoa hukumu za kisheria ambazo  baadhi yake hazieleweki.

Akizungumza na wananchi wa wilaya ya Kinondoni  wakati wa  mkutano wa kusikiliza migogoro ya ardhi kupitia Program ya Funguka kwa Waziri uliofanyika  uwanja wa shule ya msingi Bunju B jijini Dar es Salaam jana, Waziri Lukuvi alisema halmashauri kupitia kwa mwanasheria wake zinapaswa kujua maamuzi yote yanayotolewa katika Mabaraza ya Ardhi ya  Kata.

Alisema, pamoja na kilio cha wananchi wengi dhidi ya Mabaraza ya Ardhi ya Kata katika maeneo mbalimbali lakini upo utaratibu mzuri uliopangwa kuhusiana na Mabaraza hayo ingawa  yameachwa yajiendeshe yenyewe huku Halmashauri chini ya Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa ikiyaangalia bila kufuatiliwa.
 Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi akizungumza na wananchi wa wilaya ya Kiondoni mkoa wa Dar es Salaam waliojitokeza kuwasilisha migogoro yao ya ardhi  katika program maalum ya Funguka kwa waziri katika uwanja wa shule ya Msingi Bunju B.
 Mmoja wa wananchi wa Mabwepande akiwasilisha lalamiko lake la mgogoro wa ardhi kawa Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi katika program maalum ya Funguka kwa waziri katika uwanja wa Shule ya Msingi Bunju B.

  Baadhi ya wananchi waliojitokeza kuwasilisha malalamiko yao ya migogoro ya ardhi kwa Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi katika program maalum ya Funguka kwa Waziri katika uwanja wa Shule ya Msingi Bunju B.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...