Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Dkt. Bernerd Kibese (wa pili kulia) akimpongeza Mwenyekiti Mpya wa Umoja wa Mabenki Tanzania ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela baada ya kuchaguliwa kushika wadhifa huo, jana kwenye hoteli ya Serena jijini Dar es salaam. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa Umoja huo na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Standard Chartted , Sunjay Rughani, na wa pili kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Umoja wa Mabenki Tanzania, Tusekelege Mwaikasu-Jounde.
Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Dkt. Bernerd Kibese akifurahi jambo na Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa Mabenki Tanzania na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Standard Chartted , Sunjay Rughani. Katikati ni Mwenyekiti Mpya wa Umoja huo ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela 
Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Dkt. Bernerd Kibese akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Wanachama wa Umoja wa Mabenki Tanzania, baada ya kikao chao kilichofanyika jana kwenye hoteli ya Serena jijini Dar es salaam. Katika kikao hicho kulifanyika uchaguzi wa Mwenyekiti na Makamu wake ambapo, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela aliibuka mshindi na kuchukua kijiti cha Mwenyekiti wa Umoja huo, huku nafasi ya Makamu ikichukuliwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Standard Chartted , Sunjay Rughani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...