Mwenyekiti
wa UVCCM mkoa wa Songwe ndg Andrew Kadege, mapema leo amekutana na
kamati ya Utekelezaji ya wilaya ya Ileje mbali na maagizo na maelekezo
mbalimbali aliyowapa, lakini pia aliwachangia fedha taslim shilingi Laki
Tano ( 500,000/-) ili kulipia fidia ya eneo la zaidi ya ekari 20 la
UVCCM ambapo inahitajika milion 2 kulipia fidia na baadae taratibu za
kupata hati miliki zitafuata.
Ndg Kadege amesisitiza hadi januari mwishoni lazima tuwe tumemalizana na jambo la fidia kisha tuanze mchakato mapema wa kupata hati na kuanza kutekeleza mipango yetu ya kuhakikisha UVCCM tunakuwa na miradi mbalimbali na kukuza uchumi na kujitegemea ili kuepukana na hii omba omba toka kwa wadau ambao mara zote wamekuwa na masharti ya kiuchaguzi.
Pia kamati ya Utekelezaji UVCCM wilaya ya Ileje ilimpatia zawadi ya kuku kwa ajili ya Christmass.
Mwenyekiti
wa UVCCM mkoa wa Songwe ndg Andrew Kadege, akikabidhi kiasi cha
shilingi laki tano kwa kamati ya Utekelezaji ya wilaya ya Ileje ili
kulipia fidia ya eneo la zaidi ya ekari 20 la
UVCCM, ambapo inahitajika milion mbili kulipia fidia na baadae taratibu
za
kupata hati miliki zitafuata.
Mwenyekiti
wa UVCCM mkoa wa Songwe ndg Andrew Kadege akipokea Zawadi ya Jogoo wa sikukuu
kutoka kwa kamati ya Utekelezaji ya wilaya ya Ileje mara baada ya
kukutana nao mapema leo.
Mwenyekiti
wa UVCCM mkoa wa Songwe ndg Andrew Kadege akisaini kitabu cha wageni
mapema leo baada ya kukutana na kamati ya Utekelezaji ya wilaya ya Ileje





Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...