Na Agness Francis, Blogu ya Jamii
MWENYEKITI wa Taasisi ya Sekta Binafsi nchini, Salum Shamte amewataka vijana wasomi, wabunifu, wavumbuzi kutumia fursa inayotolewa na Shirika la Angel  Investors (Wawekezaji Malaika) ambalo limekuja nchini kuwafikia Watanzania kwa kutoa mitaji kwa Wafanyabiashara wadogo ili kupiga hatua.

Shamte ameyasema hayo leo Jijini Dar es Salaam katika uzinduzi maalumu wa ufunguzi wa Ofisi ya Taasisi inayohudumia Vijana ambao ni wavumbuzi, wabunifu wanaoanza biashara ambapo watasaidiwa na Taasisi ya World  Business Angel Investment  Forum (WBAF) ambayo limejikita kupeleka huduma za kifedha  kwa Vijana hao. Aidha Shamte amesema kuwa asilimia  kubwa ya vijana hapa nchini wana ukosefu wa ajira pamoja na kupata mtaji wa kujiendeleza  katika biashara.

Mkurugenzi Mkazi wa Angel Investors  Tanzania (Wawekezaji Malaika), Sabetha Mwambenja amesema kuwa tayari wamesha fanya mazungunzo na Sekta ya Umma na Binafsi ikiwamo Vyuo vya Elimu ya Juu na Ufundi, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Chuo cha Mtakatifu Joseph, Chuo Kikuu cha Tumaini, VETA, COSTECH, Taasisi yaTeknolojia Dar es Salaam (DIT), Chuo cha Kilimo cha Sokoine, (SUA), Chuo cha All Makhoum cha Mbezi Beach na  Hatamizi za Tehama (Incubators).
Mkurugenzi Mkazi wa Angel Investors  Tanzania Dkt Sabetha Mwambenja akifafanua ujio wa taasisi hiyo wakati wa ufunguzi huo wa ofisi ya WBAF hapa nchini, kuwa ni kutaka kuinua Vijana wasomi katika suala zima la kujiajiri kwa kuwawezesha namna ya kupata mtaji ili kujikwamua kiuchumi  wakati wa hafla ya ufunguzi wa ofisi hizo hapa nchini iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Sekta Binafsi Tanzania Salum Shamte akisistiza suala la Vijana waso kutumia fursa inayotolewa na Taasisi ya World Business  Angels Investment  Forum (WBAF)  lililojikita kutoa huduma za kifedha kwa Vijana wasomi, wabunifu, wavumbuzi wanaoanza biashara  kupiga hatua na kuwa wafanyabiashara wakubwa, leo katika ufunguzi wa ofisi ya taasisi ya WBAF Jijini Dar es Salaam
 Waziri wa Biashara na Maendeleo nchini Ghana Ibrahim Awal  ambaye pia ni mkulima amehudhuri ufunguzi huo wa ofisi ya WBAF hapa nchini wakati wa hafla ya ufunguzi wa ofisi hizo hapa nchini iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam..
  Mkurugenzi Mkazi  Angel Investors  Tanzania Dkt Sabetha Mwambenja (kushoto) na Mwenyekiti WBAF  Baybars Altuntas (kulia) wakionyesha mafaili kuashiria ufunguzi wa ofisi ya WBAF hapa nchini umeshakamilika leo Jijini Dar es Salaam.
Picha ya pamoja

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...