NA K-VIS BLOG
SHIRIKA la Umeme Nchini (TANESCO) limeanza operesheni ya na kuwanasa wachepusha umemeteja kadhaa eneo la Kinondoni Kaskazini.

Operesheni hiyo imeanza leo Desemba 17, 2018 ambapo wateja kadhaa wamebainika kufanya vitendo hivyo vya kuchepusha umeme ili usipite kwenye mita kwa ajili ya kufuatilia mwenendo wa matumizi yake na hivyo kuliibia Shirika.

Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari mara baada ya ukaguzi huo wa kushtukiza, Kaimu Meneja wa TANESCO anayeshughulikia wateja wakubwa, Mhandisi Frederick Njavike, alisema sio tu wateja binafsi wanaofanya hujuma hizo, lakiini pia taasisi za umma likiwemo shirika moja la umma (jina linahifadhiwa).

Mhandisi Njavike alisema kwa kawaida kila mwisho wa mwaka Shirika hupanga siku za kufanya ukaguzi wa kushtukiza ili kuangalkia sehemu gani TANESCO inapoteza mapato “Tumekuta kuna miundombinu ya TANESCO imechezewa na mbaya zaidi ni kwamba hata taasisi za umma zinashiriki vitendo hivyo, wito wetu tunaomba taasisi zote za serikali kujaribu kupitia miundombinu yote ya umeme na vile vile kuangalia watu waliowapangisha kwenye vitegauchumi vyao.” Alisema. Alisema TANESCO ni shirika la umma hivyo amewaomba wateja na wasio wateja kutoa taarifa kwa wale wote wanaochezea miundombinu kwani watakuwa wamesaidia shirika lao kuokoa fedha kutokana na wizi huo.

Wataalamu wa TANESCO wakichunguza moja ya vifaa vilivyohujumiwa ili kufanya wizi wa umeme huko Mikocheni jijini Dar es Salaam.
Kaimu Meneja wa TANESCO anayeshughulikia wateja wakubwa, Mhandisi Frederick Njavike (kulia), akizunhumza jambo na Afisa Uhusiano wa TANESCO, Bi. Samia Chande, wakati wa operesheni hiyo.

 

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...