Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetangaza uchaguzi mdogo wa kata mbili utakaofanyika tarehe 19 Januari 2019 sanjari na uchaguzi mdogo wa Jimbo la Temeke na Kata 46 za Tanzania Bara uliotangazwa awali.

Akitoa taarifa kwa umma Jijini Dar es Salaam leo (Jumanne), Makamu Mwenyekiti wa Tume, Jaji (Rufaa) Mbarouk Salim Mbarouk amezitaja kata hizo kuwa ni pamoja  na Mwanahina iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Meatu Mkoani Shinyanga  na Kata ya Biturana katika Halmashauri ya Wilaya ya Kibondo Mkoani Kigoma. 

“Fomu za Uteuzi wa Wagombea zitatolewa kati ya  tarehe  21  hadi tarehe 27, Disemba mwaka huu. Uteuzi wa Wagombea utafanyika tarehe  27, Disemba mwaka huu. Kampeni za Uchaguzi zitafanyika kuanzia tarehe 28, Disemba mwaka huu hadi tarehe 18 Januari 2019  na Siku ya Uchaguzi itakuwa ni tarehe 19  Januari 2019,” alisema Jaji Mbarouk.

Jaji Mbarouk aliongeza kwamba Uchaguzi wa Kata hizo ambao unafanyika kutokana na kujiuzulu uanachama kwa madiwani waliokuwepo awali utafanyika pamoja na uchaguzi wa Jimbo la Temeke na Kata 46 za Tanzania Bara, kama ilivyotangazwa hapo awali.

Akitoa wito kwa vyama vya siasa, Jaji Mbarouk alisema “Tume inapenda kuvikumbusha Vyama vya Siasa na wadau wote wa uchaguzi kuzingatia Sheria, Kanuni, Maadili ya Uchaguzi, Taratibu, Miongozo na maelekezo yanayotolewa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi wakati wa kipindi chote cha Uchaguzi huu mdogo”.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...