Una mpango wa kusafiri? Zingatia haya

Ni wakati mwingine tena wa msimu wa sikukuu za Krismasi na mapumziko ya mwisho wa mwaka. Katika kipindi hiki tunashuhudia pilikapilika za hapa na pale watu wakijiandaa namna watakavyosherehekea.

Kuna baadhi ya watu wanafikiria kusafiri nje ya mikoa waliyopo kwa ajili ya kusherehekea. Watu wengi wana kawaida ya kusafiri kurudi waliko zaliwa na kukulia ili kujumuika pamoja na ndugu na jamaa zao. Wengine hupanga kwenda kutembelea vivutio vya kutalii kwenye mikoa tofauti na walipo.

Kipindi cha nyuma kidogo usafiri wa umma ndio ulikuwa tegemezi ukilinganisha na sasa ambapo baadhi ya wasafiri wanamiliki usafiri wao binafsi. Kusafiri kwa usafiri binafsi kuna faida lukuki hususani kama mko wengi na wote mnakwenda sehemu moja. Hupunguza gharama lakini mnakuwa huru kuamua msafiri namna gani, muda wa kuondoka na kufika, kupumzika njiani nakadhalika.
Pamoja na faida lukuki za kusafiri kwa kutumia usafiri ubinafsi, yafuatayo ni masuala ya msingi kuyazingatia kabla ya kuanza safari yako.

Jipange mapema. Kabla ya kuanza safari yako hakikisha kuwa chombo chako cha usafiri kipo kwenye hali salama. Hali ya hewa inatofautiana kutoka mkoa mmoja kwenda mwingine hivyo huna budi kuhakikisha gari lako linakuwa na uwezo wa kuhimili hali yoyote itakayokutana nayo safarini. Wasiliana na fundi wako ambaye huwa analihudumia gari lako mara kwa mara ili kukusaidia katika hili.

Pumzika vya kutosha. Miongoni mwa sababu iliyotajwa kusahaulika kuwa inachochea kutokea kwa ajali nyingi za barabarani ni madereva kutopumzika vya kutosha kabla ya safari. Hivyo basi kama dereva ambaye unatarajia kuendesha chombo cha usafiri kwa umbali mrefu hakikisha kuwa unapata muda wa kutosha kupumzika. Hii itakusaidia mwili kuwa katika hali nzuri na kupelekea umakini mkubwa barabarani.

Kuwa makini na mwendo kasi. Hakuna haja ya kushindana kwa mwendo kasi na madereva wengine barabarani. Zingatia umbali wa kutosha baina yako na chombo kingine cha usafiri ili kuweza kuepuka ajali pindi itakapotokea. Takwimu tofauti duniani zinaonesha kuendesha gari kwa mwendo kasi kunapelekea ajali nyingi, majeruhi wengi na hata vifo zaidi. Unashauriwa kuendesha kwa kuzingatia alama za barabarani.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>>>

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...