Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

RAIS wa Serikali ya Awamu ya Tano Dk.John Magufuli amewataka Watanzania kuendelea kufanya kazi kwa bidii na kuacha kulalamika kuwa vyuma vimebana kwani ukifanya kazi chuma hakitakubana bali utavibanua.

Ametoa kauli hiyo leo jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa ujenzi wa barabara inayoanzia Kimara hadi Kibaha mkoani Pwani ambapo Rais aliamua pia kuzungumzi wanaolalamika vyuma kukaza.

"Tusilalamike vyuma vimebana kwani ukifanya kazi vyuma hakitakubana utavibanua.Sasa watu watu wanatumia maneno ya kawaida vyuma vinabana kila wakati utasikia wanasema vyuma vimebana .Lazima niwaambie ukweli usipofanya kazi vitabana kweli kweli hadi utachoka mwenyewe, hakuna vya bure...

"Huo ndio ukweli ninafuu niwaeleze hata kwenye maandiko matakatifu yanasema asiyefanya kazi na asile na usipokula utakufa.Eti hakuna atakayekufa na njaa.Mimi nawaambia usipofanya kazi utakufa njaa kwani hakuna hakua vya bure.Hili la vyuma kukaza ni mambo ya siasa tu na bahati nzuri Watanzania wameshaelewa sana.

Wakati huo huo Rais Magufuli amesema kuwa hii seriakali si katali ila ni sehemu ya maendeleo ya watanzania, hivyo amewaomba Watanzania wa vyama vyote kujiamini kwamba tunaweza japo kwa miaka mitano na atakapomaliza muda wake waendelee na 
kutojiamini."Watazania tumechezewa na tumeliwa mno".
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihotubia Wananchi katika hafla ya uwekaji jiwe la Msingi la Ujenzi wa Upanuzi wa barabara ya Morogoro Kuanzia Kimara hadi Kibaha yenye Urefu wa Kilometa 19.2 .Hafla iliyofanyika Kimara Jijini Dar es Salaam Desemba 19, 2018.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...