Wizara ya Afya Idara Kuu Maendeleo ya Jamii inakutana na wadau wa masuala ya Jinsia kujadiliana na kufanya mapitio ya sera ya Taifa ya Jinsia ili pamoja na mambo mengine iweze kuwa na masuala ya wanawake waishio vijijini lakini pia kuzingatia makundi mengine maalumu hususani vijana na watu wenye mahitaji maalum.
Akiongea wakati wakufungua kikao kazi na wadau wa sera ya jinsia kutoka Wizara za serikali na mashirika yasiyo ya Kiserikali Kaimu Mkurugenzi wa Jinsia kutoka Wizara ya Afya Idara kuu Maendeleo ya Jamii Bi Grace Mbwilo amewataka wadau hao kufanya mapitio ya sera hiyo lakini pia kuangalia namna bora ya kutatua changamoto zinazomkabili mwanamke wa kijijini.
Aidha Bi. Mbwiro pia amewataka wadau hao kuangalia masuala mengine katika jamii akisema ni mengi mno hivyo kuzingatia vipaumbele vya masuala ya jinsia kwa wanawake akisema kundi hilo katika jamii bado linachangamoto ambazo zinalifanya kuendelea kubaki katika nyanja tofauti.
Kaimu Mkurugenzi Idara ya Jinsia kutoka Wizara ya Afya Idara Kuu Maendeleo ya Jamii Bi Grace Mbwilo katikati akiongea na wadau mbalimbali wa masuala ya Jinsia wakati wa kujadiliana na kufanya mapitio ya sera ya Taifa ya Jinsia leo Mkoani Morogoro.
Wadau mbalimbali wa masuala ya Jinsia wakati wa kujadiliana na kufanya mapitio ya sera ya Jinsia katika kikao kikazi cha wadau wadau wa Jinsia kinachoratibiwa na Wizara ya Afya Idara Kuu Maeandeleo ya Jamii leo Mkoani Morogoro.
Wadau mbalimbali wa masuala ya Jinsia wakati wa kujadiliana na kufanya mapitio ya sera ya Jinsia katika kikao kikazi cha wadau wadau wa Jinsia kinachoratibiwa na Wizara ya Afya Idara Kuu Maeandeleo ya Jamii leo Mkoani Morogoro.
Baadhi ya wadau mbalimbali wa masuala ya Jinsia wakati wa kujadiliana na kufanya mapitio ya sera ya Jinsia katika kikao kikazi cha wadau wadau wa Jinsia kinachoratibiwa na Wizara ya Afya Idara Kuu Maeandeleo ya Jamii leo Mkoani Morogoro.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...