MSANII maarufu katika muziki wa kizazi kipya nchini Nasseb Abdull a.k.a Diamond ameahidi kuwasaidia wanamuziki wa taarab nchini huku akitoa onyo kwa wale wasanii ambao wanatoa fedha ili nyimbo zao zipigwe kwenye redio na Televisheni ya Wasaf.
Diamond ametoa kauli hiyo leo wakati anazungumza mbele ye Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda ambaye ameamua kuwaita wasanii wa tasnia mbalimbali kuzungumza nao.
Amesema amesikia anatambua nafasi ya wasanii kushirikiana na kusaidiana katika kuhakikisha kazi zao za sanaa zinasonga mbele, hivyo ametumia nafasi hiyo kuahadi nyimbo za taraab kupigwa kwenye Redio ya Wasaf pamoja na Wasaf TV.
“Nimesikia mama yangu Khadija Kopa amezungumzia kuhusu muziki wa taarab, naomba nimwambie nyimbo za taarab tutazipiga bila tatizo lolote, tunaomba watuleteee tu.
“Pia naomba niseme hapa kuna wasanii ambao wanatoa fedha Wasaf ili nyimbo zao zipigwe.Hili sitaki kuona likienda na msanii nikisikia analeta fedha kwa ajili ya nyimbo yake ipigwe nitamfungia,”amesema Diamond.
Amefafanua lengo la kuanzisha Wasafi TV na Wasaf FM ni kuwasaidia wasanii wote na hivyo hataki kusikia habari ya msanii kutoa rushwa ili nyimbo zake zipigwe.




Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...