Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Waziri Mkuu na Bunge), Bi. Maimuna Tarishi akishuhudia makabidhiano rasmi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Katibu Mkuu mpya (Sera na Uwekezaji), Bi. Dorothy Mwaluko kutoka kwa aliyekuwa Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Profesa, Faustin Kamuzora ambaye ameteuliwa hivi karibuni kuwa Katibu Tawala mkoani Kagera. Katibu Mkuu Mwaluko kabla ya uteuzi huo alikuwa Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Menejineti ya Utumishi wa Umma na Utawala bora
Aliyekuwa Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu), Profesa, Faustin Kamuzora akishukuru kwa ushirikiano aliokuwa anapewa wakati akihudumu katika ofisi hiyo, kwa Katibu Mkuu (Waziri Mkuu na Bunge), Bi. Maimuna Tarishi (katikati) na Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uwekezaji), Dorothy Mwaluko (kushoto )
Aliyekuwa Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu), Profesa, Faustin Kamuzora akiwa katika picha ya pamoja na waliokuwa Makatibu Muhtasi wake, pamoja na Katibu Mkuu mpya Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uwekezaji), Dorothy Mwaluko (kulia), mara baada ya Profesa Kamuzora kumkabidhi ofisi rasmi. Picha na PMO
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...