Na Abdullatif Yunus - Kagera

Kutokana na ukosefu wa huduma ya Maji katika baadhi ya maeneo Nchini, ambayo miradi ya Maji kuharibiwa na kuhujumiwa na Majangili wa miundo mbinu ya Maji, Naibu Waziri wa Maji Jumaa Aweso ameagiza Viongozi kuweka Ulinzi madhubuti kwa ajili ya kulinda wahujumu hao na pindi watakapobainika sheria ifuate mkondo wake.

Akiwa katika ziara ya Kikazi Wilayani Ngara jana Januari 12,2019, Naibu Waziri Aweso amesema Serikali imekuwa ikiwekeza pesa nyingi kwa miradi mbalimbali ya Maji hapa Nchini, lakini miundo mbinu ya miradi hiyo imekuwa ikiharibiwa na wakati mwingine kuibwa na wale alowaita Majangili wa Maji.

 Katika ziara hiyo Naibu Waziri Aweso ametembelea mradi wa Maji unaosukumwa kwa Nishati ya Umeme unaohudumia Vijiji vya Muhweza na Murugarama. Mradi huo Ulioanza Mwaka 2014, ni miongoni mwa Vijiji 10  chini ya programu ya Sekta ya Maji (WSDP) wenye gharama zaidi ya Shilingi Milioni 559.
 Pichani ni Mtoto Zainabu Mohammed Mkazi wa Muhweza akisuuza Ndoo kabla ya  Maji kama alivyokutwa na Kamera yetu.
 Pichani ni Bi. Zubeda Baraka Mkazi wa Muhweza Wilayani Ngara, akifurahia huduma ya Maji iliyosogezwa karibu baada ya kuteseka kwa muda  kufuata Maji umbali mrefu.
 Tanki la Maji la Mradi wa Vijiji vya Muhweza na Murugarama unaoendelea kujengwa na Unatarajiwa kuzinduliwa Machi mwaka huu unaogharimu zaidi ya Shilingi Milioni 559.
 Pichani Mh. Aweso akiwa juu ya Tanki la Maji linaloendelea kujengwa likiwa katika hatua za mwisho licha ya kuanza kuhudumia mradi huo.
Mh. Aweso Naibu Waziri wa Maji akinawa mkono katika Tanki kwenye mradi wa Maji wa Muhweza - Murugarama alipotembelea mradi huo mapema Januari 12, 2019.
index
Naibu Waziri wa Maji Mh. Jumaa Aweso (MB) akishiriki kazi ya kutandaza mabomba ya maji katika mradi huo unaotekelezwa katika vijiji vya  Kabalenzi-Kanazi
index
Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso akizungumza na Kaimu Mhandisi wa Wilaya ya Ngara, Simon Ndyamukama kuhusu utekelezaji wa Mradi wa Maji wa Kabalenzi-Kanazi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...