Dr N T Jiwaji (Mwenyekiti ASSAT) 11 Januari 2019 

 Mwaka huu 2019 Muungano wa Kimataifa wa WanaAstronomia (International Astronomical Union – IAU) unasheherekea miaka mia tangu uundwe (1919-2019), ili kuunganisha nguvu za wanaAstronomia wa kila sehemu ya Dunia kuunganika kuchunguza, kuelewa na kuendeleza fani ya Astronomia kwa ajili ya kufaidi matokeo yake.

Hapa Tanzania tunausheherekea mwaka huu kama shughuli za MIAKA 100 YA ASTRONOMIA zikiongozwa na Chama cha Astronomia na Sayansi ya Anga Tanzania (Astronomy and Space Science Association of Tanzania – ASSAT) katika makao yake Chuo Kikuu Huria cha Tanzania na leo tarehe 11 Januari 2019 tuna zindua sherehe hizo.

Matukio mbalimbali ya kimataifa yameandaliwa na IAU katika kuusheherekea mwaka. MASAA 100 YA ASTRONOMIA ni mojawapo ya shughuli ambapo wanaastronomia Duniani kote wanahamashisha jamii wakiwemo watoto, wanafunzi, waalimu, wafanyakazi, vijana, wazee na wote kwa ujumla kuelewa na kufurahia na kushughulika katika mambo ya Astronomia na kuelewa sayansi ya asili.

Masaa 100 hayo ni kuanzia tarehe 11 hadi 14 Januari ambapo mamilioni ya watu wanaalikwa kutazama angani kwa macho au kwa kutumia darubini na kuangalia, kufurahia na kuelewa maajabu ya Ulimwengu wetu.  Anga ni moja hiyo hiyo kwa watu wote Duniani na ndio inatuunganisha binaadamu wote.

Leo hii tarehe 11 January 2019, Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kimepanga tukio hili kuzindua shughuli zetu za MIAKA 100 YA ASTRONOMIA na kualika watu washiriki kwa pamoja katika MASAA 100 YA ASTRONOMIA kwa kuangalia anga.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...