Na Ripota Wetu,Globu ya jamii

JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limesema Jiji hilo liko shwari na hakuna tukio lolote la uvunjifu wa amani ambalo linahusishwa na uwepo wa 'Panya road'.

Akizungumza leo, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam Lazaro Mambosasa amewahakikishia wananchi wa Jiji hilo kuwa hali ni shwari na hakuna tukio ambalo limetokea hasa kwenye siku ya mkesha wa mwakya mpya wa 2019.

"Tumeona moja ya gazeti likisema 'Panya road watikisa Dar'.Ukweli hakuna tukio limehusisha panya road siku ya mkesha wa mwaka mpya.Dar iko salama sana , hivyo taarifa hizo hazina ukweli wowote,"amesema Kamanda Mambosasa na kusisitiza Jeshi la Polisi Kanda Maalum limejipanga kuhakikisha usalama upo wa kutosha.

Amefafanua katika siku ya mkesha wa mwaka mpya kulikuwa na makundi ya watu mbalimbali wakiwamo wanaosheherekea mwaka mpya,makundi ya watu waliotoka Kanisani na maeneo mengine, hata hivyo hakukuwa na tukio ambalo limefanywa na hao wanaodaiwa kuwa panya road kwani hakuna panya road .

"Tupo kwa ajili ya kuhakikisha hali ya usalama inakuwa salama,hivyo asitokee mtu mmoja kwa utashi wake awatia hofu wananchi kwa kudai kuna panya road wakati hakuna," amesema Kamanda Mambosasa na kuongeza kuwa wananchi wasiwe na hofu na kuwatataka waendelee na shughuli zao kama kawaida za ujenzi wa uchumi wao na Taifa kwa ujumla kwa mwaka huu wa 2019.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...