MKUU
wa Mkoa wa Manyara, Alexander Pastory Mnyeti ameagiza wachimbaji wadogo
wa madini ya Tanzanite (WanaApolo) wapite bila kulipa kwenye lango la
kuingia ndani ya ukuta unaozunguka migodi ya madini hayo hadi hapo
utaratibu wa kulipia sh70,000 ili wapatiwe vitambulisho vya kupita
utakapofanyika.
Uamuzi
huo umepokelewa kwa mikono miwili na wananchi wa mji mdogo wa Mirerani
kwani awali waliokuwa wanaruhusiwa ni wale wenye mkataba wa kulipwa
mshahara pekee.
Mnyeti
akizungumza na wadau wa madini alisema wanaApolo watapita bila kulipa
chochote kwenye lango hilo hadi hapo vitambulisho maalum
vitakapoandaliwa ambavyo watalipia kila mmoja sh70,000 kwa mwaka mmoja. Alisema
wamekubaliana kwenye kikao cha wamiliki wa migodi na wanaApolo kuwa
suala la malipo ya mishahara au asilimia 10 pindi madini yakitoka
wataamua wao wenyewe.
"Baada
ya serikali kukubaliana na pendekezo lenu la kuachana na suala la
mishahara ambalo lipo kisheria inabidi ikusanye kodi ya mshahara na tozo
ya uendelezaji ufundi stadi," alisema Mnyeti. Mbunge wa jimbo la Simanjiro James Ole Millya alisema wanamshukuru Mnyeti kwa uamuzi huo kwani utawanufaisha watu wengi.
Aliwataka
wamiliki wa migodi na wachimbaji wote kutimiza wajibu wao huku
wakitilia mkazo suala la ulipaji wa kodi kwa ajili ya maendeleo.Mwenyekiti
wa chama cha wachimbaji madini mkoa wa Manyara, (Marema) Justin Nyari
alisema Mnyeti ameweka historia kwa tamko hilo kwani baadhi ya
wachimbaji waliondoka ila sasa watarudi.
Nyari
alisema wao kama viongozi wa wachimbaji watakutana na makundi yote
yanayojihusisha na madini hayo ili kuweka utaratibu mzuri wa kufanya
shughuli hiyo na wanaApolo kutohama hama. Katibu
wa Marema tawi la Mirerani, Omary Mandari alisema wanampongeza Rais
John Magufuli kwa kujenga ukuta huo na mkuu wa mkoa kwa uamuzi wake wa
kuruhusu watu kupita.
Mandari
alisema utaratibu huo wa kuingia bila malipo wakati huu ikisubiriwa
vitambulisho maalum ni mzuri tofauti na hapo awali ambapo wanaApolo
ilitakiwa waingie kwa kutumia mikataba ya mishahara. Makamu
Mwenyekiti wa usalama, afya na mazingira wa shirikisho la wachimbaji
madini nchini (Femata) Dk Bernard Joseph alisema wamejipanga kuhakikisha
utunzaji mazingira na afya za wafanyakazi.
Dk
Joseph alisema wameweka utaratibu wa wafanyakazi wanaofanya shughuli
migodini ikiwemo kuumia, uokoaji na kufukiwa tukishirikiana na
wachimbaji wazoefu na Wizara ya Madini.
Mkuu
wa Mkoa wa Manyara, Alexander Pastory Mnyeti akipokelewa na askari wa
Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na polisi kwenye geti la Magufuli
la kuingia ndani ya ukuta unaozunguka migodi ya madini ya Tanzanite Mji
mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro.
Mwenyekiti
wa chama cha wachimbaji madini Mkoa wa Manyara (Marema) Justin Nyari
akizungumza kwenye kikao cha wadau wa madini ya Tanzanite Mji mdogo wa
Mirerani Wilayani Simanjiro.
Mkuu
wa kituo cha polisi Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, ASP
Evarest Makala akielezea mikakati ya ulinzi na usalama.
Mkuu
wa Mkoa wa Manyara Alexander Pastory Mnyeti akizungumza kwenye kikao
cha wadau wa madini ya Tanzanite Mji mdogo wa Mirerani Wilayani
Simanjiro.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...