MKUU wa Wilaya ya Mbulu Mkoani Manyara, Chelestino Mofuga amezindua ugawaji wa vitambulisho vya wafanyabiashara wadogo kwa kwa kuwataka watumishi wanaosimamia zoezi hilo kutowapa usajili wafanyabiashara wakubwa.

Wafanyabiashara wadogo 5,000 wanatarajia kupata vitambulisho hivyo wilayani Mbulu ambapo kwa kuanzia wamegawa vitambulisho 1,008 kati ya 2,500 vinavyotolewa kwa awamu ya kwanza.

Mkuu wa wilaya ya hiyo, Chelestino Mofuga aliyasema hayo wakati akizindua zoezi la ugawaji vitambulisho kwa wafanyabiashara wadogo wa Mbulu mjini, Haydom na Dongobesh. Mofuga aliwaagiza mkurugenzi wa mji wa Mbulu, Anna Mbogo na mkurugenzi wa halmashauri hiyo, Hudson Kamoga kuhakikisha zoezi hilo linawanufaisha wahusika pekee.

Alisema zoezi hilo linapaswa kufanyika kwa umakini mno ili kuepuka kuwasajili wafanyabiashara wakubwa jambo linaloweza kushusha mapato ya serikali. "Msikiuke maagizo ya Rais John Magufuli aliyotoa wakati anakabidhi vitambulisho hivi aliagiza viwanufaishe wafanyabiashara ambao mauzo yao hayazidi sh4 milioni kwa mwaka," alisema Mofuga.
Mkuu wa Wilaya ya Mbulu Mkoani Manyara, Chelestino Simbalimile Mofuga akipeana mkono baada ya kumkabidhi kitambulisho mfanyabiashara wa mji mdogo wa Haydom, James Boay. 
 Mkuu wa Wilaya ya Mbulu Mkoani Manyara, Chelestino Simbalimile Mofuga akiongoza kikao cha kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya na wasimamizi wa zoezi la ugawaji vitambulisho kwa wafanyabiashara wadogo.
 Mkuu wa Wilaya ya Mbulu Mkoani Manyara, Chelestino Simbalimile Mofuga akizungumza na wafanyabiashara wadogo watakaopatiwa vitambulisho vinavyotolewa na Rais John Magufuli.
 Baadhi ya wafanyabiashara wadogo wa wilaya ya Mbulu mkoani Manyara wanatarajia kupatiwa vitambulisho vilivyotolewa na Rais John Magufuli. 

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>>>

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...