Na Ripota Wetu, Globu ya jamii 

MSANII Bi Kidide amemuomba Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda kuwa amekuwa katika sanaa kwa zaidi ya miaka 25 lakin hakuna ambacho amenufaika nacho na hivyo anamuomba amsaidie. 

Ametoa kauli hiyo leo wakati Makonda alipokutana na wasanii wa fani mbalimbali kwa lengo la kujadiliana nao mambo mbalimbali yanayohusu sanaa. 

“Mkuu wangu wa Mkoa wa Dar es Salaam naomba nikwambie tu nipo kwenye sanaa kwa miaka 25 sasa lakini hakuna ambacho nimenufaika nacho.Naomba unisaidie name mambo yawe sawa,”amesema Bi. Kidide. 

Bi Kidide pia amemuomba Makonda kuhakikisha wasanii wanapata bima ya afya ambayo ni muhimu kwa wasanii wa tasnia mbalimbali.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...