Na Ripota Wetu, Globu ya jamii 

MWANAMUZIKI  maarufu katika Muziki wa Taarab nchini Khadija Kopa amesema anasikitishwa na kitendo cha wasanii wa muziki huo kutopewa kipaumbele kama ilivyo kwa wasanii wengine wakiwamo wa Bongo Fleva na waigizaji filamu. 

Kopa amesema hayo leo katika viwanja vya Leaders jijini Dar es Salaam baada ya Makonda kuamua kukutana na wasanii wa fani mbalimbali. 

“Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam naomba niseme umenigusa sana kwenye hili la wasanii kuwa wamoja. Ni jambo muhimu kwa wasanii kuwa na umoja imara.Umoja ambao unazungumziwa uwe wa wasanii wote bila ya kuwapo ubaguzi. 

“Nitoe kilio changu hasa kwa Serikali, wanamuziki wa taarab wanakufa lakini hakuna hata ushiriki wa Serikali wakati akitoa msanii wa muziki wa Bongo Fleva au waigizaji wa filamu wanathaminiwa na tunaona.Hivyo nitoe rai nasi tunastahili kuthaminiwa na kushirikishwa katika mambo mbalimbali,”amesema Kopa. 

Amefafanua anashindwa kuelewa namna ambavyo jamii inawachukulia wanamuziki wa taarabu nchini”Sijui wanamuziki wa taarab tunaonekana ni watu maskini sana au sijui kuna nini?Tunastahili kuthaminiwa.” 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...