NA ALFRED MGWENO TEMESA
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle amefanya ziara katika mikoa ya Arusha na Kilimanjaro na kuwataka wafanyakazi wa Wakala huo katika mikoa hiyo kuongeza juhudi katika kazi ili kuhakikisha wanazalisha kipato cha kutosha kuweza kufikia malengo au hata kuzidi mapato waliyojiwekea kwa mwaka huu wa fedha wa 2018/2019.
Akizungumza na wafanyakazi hao kwa nyakati tofauti, Mhandisi Maselle alisema anatambua kwamba TEMESA inakumbwa na changamoto nyingi za kiutendaji ikiwemo ukosefu wa vifaa vya kutendea kazi hasa vya karakana pamoja na upungufu wa wafanyakazi lakini aliwataka mameneja wa mikoa hiyo pamoja na watumishi wake kujitahidi kufanya kazi zao kwa ufansi na kwa ushirikiano huku akiangalia namna ya kuwaongezea vitendea kazi na kujaza nafasi za watumishi zilizoachwa wazi baada ya kustaafu.
Katika mazungumzo yake Mhandisi Maselle alisisitiza kwamba, Kiongozi mzuri ni yule ambaye anafanya kazi bega kwa bega na wafanyakazi wenzake pale anapoona mapungufu na kuwatia moyo hivyo meneja ajitahidi kuwa karibu na watumishi wake.
Mtendaji
Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle
(kulia) akikagua mashine ya kuchongea vipuri vya injini za magari katika
karakana ya TEMESA mkoa wa Kilimanjaro wakati wa ziara yake mkoani humo
kukagua utendaji kazi na kusikiliza kero mbalimbali zinazowakabili
wafanyakazi wa wakala huo. Kushoto ni Meneja wa Temesa mkoani humo
Mhandisi Ferdinand Mishamo.
Mtendaji
Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle
(kulia) akitoa maelekezo wakati akikagua mashine ya kubadilishia tairi
za magari katika karakana ya TEMESA mkoa wa Kilimanjaro alipotembelea
kujionea utendaji kazi na kusikiliza kero mbalimbali zinazowakabili
wafanyakazi wa wakala huo. Kushoto ni Meneja wa TEMESA mkoani humo
Mhandisi Ferdinand Mishamo.
Mtendaji
Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle
(kushoto) akitoa maelekezo kwa mafundi na wafanyakazi wa karakana ya
mkoa wa Arusha mara baada ya kukagua mtambo wa kuchenjua na kuchakata
kokoto (Crusher) unaoonekana pichani.
Mtendaji
Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle
katikati (aliyevaa koti) akikagua mitambo mbalimbali iliyopo katika
karakana ya wakala huo mkoani Arusha.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...