SHIRIKA la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF)
imeanza utekelezaji wa maagizo ya Rais Dk.John Magufuli aliyoyatoa
katika mkutano kati ya viongozi wa vyama vya wafanyakazi, Mamlaka ya
Usimamizi na Udhibiti wa sekta ya Hifadhi ya jamii(SSRA), watendaji
wakuu wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii na Chama cha waajiri uliofanyika
Desemba 28, 2018 Ikulu jijini Dar es salaam.
Taarifa ya NSSF kwa vyombo vya habari iliyotolewa jana Januari 6,2019 imesema Mfuko unaendelea kupokea na kuhakiki madai mbali mbali kutoka kwa wanachama ambao ajira zao zimekoma na walikuwa kwenye ajira za muda maalumu kwenye sekta mbali mbali kama vile madini, viwanda, ujenzi na kilimo.
Imesema madai yote yanayothibitishwa kuwa ni halali baada ya kuhakikiwa, mwanachama atalipwa mafao yake. Meneja Kiongozi wa Matekelezo (Chief Manager Compliance and Data Management ) Cosmas Sasi amesema NSSF inaendelea kulipa mafao mbali mbali kwa wanachama wake kwa wakati. Kwa upande wa mafao ya uzeeni takribani Sh. bilioni 5 zimekuwa zinalipwa kila mwezi kwa wastaafu wetu kuanzia julai 2018.Wakati kwa pensheni ya Desemba,2018 Sh. Bilioni 4.83 kimeshalipwa kwa wastaafu 18,631 walikuwepo kwenye daftari la wastaafu.
Kwa upande wa malimbikizo ya mafao hadi kufikia julai 2018 jumla ya Sh. bilioni 108 zilikuwa zinadaiwa kwenye Shirika, ambapo kiasi cha Sh. bilioni 85 kimelipwa kwa wanachama waliokuwa na madai mbali mbali baada ya uhakiki kukamilika, kiasi kilichobaki cha sh. bilioni 23 kitalipwa baada ya uhakiki unaondelea kukamilika.
Wakati huo huo Meneja Kiongozi Uhusiano na Elimu kwa UmaLulu Mengele amesema Mfuko ulianza mchakato wa kuhakiki wastaafu wake kuanzia Desemba 1, 2018 na bado unaendelea kwenye ofisi mbali mbali za NSSF zilizoko mikoa yote ya Tanzania Bara ."Wastaafu ambao hawajajitokeza kuhakiki, wanaombwa wafike kwenye ofisi zetu 65 zilizoko katika maeneo mbali mbali katika mikoa yote Tanzania bara kwa upande wa wastaafu wanaoishi Zanzibar watahakikiwa kwenye ofisi za ZSSF.
Taarifa ya NSSF kwa vyombo vya habari iliyotolewa jana Januari 6,2019 imesema Mfuko unaendelea kupokea na kuhakiki madai mbali mbali kutoka kwa wanachama ambao ajira zao zimekoma na walikuwa kwenye ajira za muda maalumu kwenye sekta mbali mbali kama vile madini, viwanda, ujenzi na kilimo.
Imesema madai yote yanayothibitishwa kuwa ni halali baada ya kuhakikiwa, mwanachama atalipwa mafao yake. Meneja Kiongozi wa Matekelezo (Chief Manager Compliance and Data Management ) Cosmas Sasi amesema NSSF inaendelea kulipa mafao mbali mbali kwa wanachama wake kwa wakati. Kwa upande wa mafao ya uzeeni takribani Sh. bilioni 5 zimekuwa zinalipwa kila mwezi kwa wastaafu wetu kuanzia julai 2018.Wakati kwa pensheni ya Desemba,2018 Sh. Bilioni 4.83 kimeshalipwa kwa wastaafu 18,631 walikuwepo kwenye daftari la wastaafu.
Kwa upande wa malimbikizo ya mafao hadi kufikia julai 2018 jumla ya Sh. bilioni 108 zilikuwa zinadaiwa kwenye Shirika, ambapo kiasi cha Sh. bilioni 85 kimelipwa kwa wanachama waliokuwa na madai mbali mbali baada ya uhakiki kukamilika, kiasi kilichobaki cha sh. bilioni 23 kitalipwa baada ya uhakiki unaondelea kukamilika.
Wakati huo huo Meneja Kiongozi Uhusiano na Elimu kwa UmaLulu Mengele amesema Mfuko ulianza mchakato wa kuhakiki wastaafu wake kuanzia Desemba 1, 2018 na bado unaendelea kwenye ofisi mbali mbali za NSSF zilizoko mikoa yote ya Tanzania Bara ."Wastaafu ambao hawajajitokeza kuhakiki, wanaombwa wafike kwenye ofisi zetu 65 zilizoko katika maeneo mbali mbali katika mikoa yote Tanzania bara kwa upande wa wastaafu wanaoishi Zanzibar watahakikiwa kwenye ofisi za ZSSF.
Meneja Kiongozi wa Matekelezo ,Cosmas Sasi Kutoka Shirika NSSF,akizungumza na
Waandishi wa habari (hawapo pichani) jana jijini Dar kuhusu namna
ambavyo NSSF
imeanza utekelezaji wa maagizo ya Rais Dk.John Magufuli aliyoyatoa
katika mkutano kati ya viongozi wa vyama vya wafanyakazi, Mamlaka ya
Usimamizi na Udhibiti wa sekta ya Hifadhi ya jamii (SSRA), watendaji
wakuu wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii na Chama cha waajiri uliofanyika
Desemba 28, 2018 Ikulu jijini Dar es salaam.
Sasi alisema kuwa NSSF ilianza mchakato wa kuhakiki wastaafu wake kuanzia Desemba 1, 2018 na bado unaendelea kwenye ofisi mbali mbali za NSSF zilizoko mikoa yote ya Tanzania Bara ."Wastaafu ambao hawajajitokeza kuhakiki, wanaombwa wafike kwenye ofisi zetu 65 zilizoko katika maeneo mbali mbali katika mikoa yote Tanzania bara kwa upande wa wastaafu wanaoishi Zanzibar watahakikiwa kwenye ofisi za ZSSF",alisema.Pichani kulia ni Meneja Kiongozi Uhusiano na Elimu kwa Uma,Lulu Mengele
Meneja
Kiongozi Uhusiano na Elimu kwa Uma,Lulu Mengele akizunguma na
Waandishi wa habari (hawapo pichani) jana jijini Dar akifafanua kuhusu
uhakiki wa Wananchama wao,Lulu alisema kuwa Mfuko wa NSSF unaendelea kupokea na kuhakiki madai mbali mbali kutoka kwa wanachama
ambao ajira zao zimekoma na walikuwa kwenye ajira za muda maalumu
kwenye sekta mbali mbali kama vile madini, viwanda, ujenzi na kilimo.
"Madai yote yanayothibitishwa kuwa ni halali baada ya kuhakikiwa, mwanachama atalipwa mafao yake. kwa hiyo NSSF kwa sasa inaendelea kulipa mafao mbali mbali kwa wanachama wake kwa wakati,",alisema Lulu.Pichani kushoto ni Meneja Kiongozi wa Matekelezo ,Cosmas Sasi Kutoka Shirika NSSF.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>>
"Madai yote yanayothibitishwa kuwa ni halali baada ya kuhakikiwa, mwanachama atalipwa mafao yake. kwa hiyo NSSF kwa sasa inaendelea kulipa mafao mbali mbali kwa wanachama wake kwa wakati,",alisema Lulu.Pichani kushoto ni Meneja Kiongozi wa Matekelezo ,Cosmas Sasi Kutoka Shirika NSSF.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>>
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...