Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Dkt. James Kilaba akiwa kapigwa na butwaa na baadaye kushukuru wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli alipomhakikishia kumwongeza mkataba wa miaka mitano kuongoza taasisi hiyo katika hafla ya makabidhiano ya Mfumo wa Kudhibiti Mawasiliano ya Ndani na Nje ya Nchi (TTMS) iliyofanyika makao Makuu ya TCRA Jijini Dar es salaam leo Januari 18, 2019.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia katika hafla ya makabidhiano ya Mfumo wa Kudhibiti Mawasiliano ya Ndani na Nje ya Nchi (TTMS) iliyofanyika makao Makuu ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Jijini Dar es salaam leo Januari 18, 2019.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na viongozi
wengine meza kuu wakimsikiliza Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai akiongea
machache wakati wa hafla ya makabidhiano ya Mfumo wa Kudhibiti
Mawasiliano ya Ndani na Nje ya Nchi (TTMS) iliyofanyika makao Makuu ya
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Jijini Dar es salaam leo Januari
18, 2019.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na viongozi wengine wakipata picha ya kumbukumbu na viongozi wa dini katika hafla ya makabidhiano ya Mfumo wa Kudhibiti Mawasiliano ya Ndani na Nje ya Nchi (TTMS) iliyofanyika makao Makuu ya TCRA Jijini Dar es salaam leo Januari 18, 2019.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli aakipeana mikono na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Dkt. James Kilaba katika hafla ya makabidhiano ya Mfumo wa Kudhibiti Mawasiliano ya Ndani na Nje ya Nchi (TTMS) iliyofanyika makao Makuu ya TCRA Jijini Dar es salaam leo Januari 18, 2019.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipeana mikono na Askofu Mkuu wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF) Zacharia Kakobe katika hafla ya makabidhiano ya Mfumo wa Kudhibiti Mawasiliano ya Ndani na Nje ya Nchi (TTMS) iliyofanyika makao Makuu ya TCRA Jijini Dar es salaam leo Januari 18, 2019.
Makabidhiano ya Mfumo wa Kudhibiti Mawasiliano ya Ndani na Nje ya Nchi (TTMS) baina ya wakandarasi Bw. James Gabriel Claude CEO wa kampuni ya GVG na Samuel Kiki Gyan Mkurugenzi wa kampuni ya SGS na Mkurugenzi Mkuu wa TCRA Dkt. James Kilaba katika hafla iliyofanyika makao Makuu ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Jijini Dar es salaam leo Januari 18, 2019.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na
viongozi wengine akiwasili katika hafla ya makabidhiano ya Mfumo wa
Kudhibiti Mawasiliano ya Ndani na Nje ya Nchi (TTMS) iliyofanyika makao
Makuu ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Jijini Dar es salaam leo
Januari 18, 2019.
PICHA NA IKULU
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...