Na Ripota, BBC 

RAIS wa nchi ya Gabon Ali Bongo ameamua kurejea nchini kwake ikiwa ni moja tu tangu kufanyika kwa jaribi la kimapinduzi la kutaka kumuondoa madarakani.

Bongo mwenye umri wa miaka 59 amerejea nchini mwake akitoa nchini Morocco ambapo alikuwa amekwenda kwa ajili ya kupatiwa matibabu na amekaa nchini humo kwa miezi miwili.Hivyo amerejea nchini kwake baada ya jeshi kufanikiwa kuzima jaribio la mapinduzi ya Serikali yake.Rais huyo akiwa kwenye mkutano mkuu wa kiuchumi nchini Saudi Arabia alipatwa na Kiharusi.

Taarifa kuhusu Rais Ali Bongo ambayo imetolewa leo Januari 15,2019 na Shirika la Habari la Uingereza(BBC) inaeleza kuwa kwa sasa yupo nchini kwake.Rais huyo baada ya kuwepo kwa utata kuhusu hali yake Desemba mwaka jana aliamua kutangaza kupatwa na kiharusi.

Kwa mujibu wa BBC ni kwamba wiki iliyopita, jeshi nchini humo lilizima jaribio la mapinduzi ya Serikali na kumkamata kiongozi wa kundi hilo na pia kuwaua wanajeshi wawili waliokuwa wamevamia kituo cha redio ya taifa.

Inaelezwa wanajeshi hao walisema walihisi hotuba ya Bw Bongo ya Mwaka ilidhihirisha kwamba kiongozi huyo alikuwa amepoteza uwezo wake wa kuliongoza taifa hilo.Mwishoni mwa wiki, Waziri Mkuu Julien Nkoghe Bekale alitangaza mabadiliko katika baraza la mawaziri.Katiba ya Gabon inasema mawaziri ni lazima wale kiapo mbele ya Rais.
RAIS wa nchi ya Gabon Ali Bongo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...