NA TIGANYA VINCENT, TABORA
SERIKALI Wilayani Uyui imesema inakusudia kuendesha Kampeni maalumu ya Nishike Mkono Mwezi Machi mwaka huu kwa lengo la kukusanya shilingi bilioni 1.5 (1,500,000,000/-) ambazo zitasaidia ujenzi wa dahari(hosteli) 15 kwenye Sekondari 15 za Kata ili kuwalinda watoto wa kike na mimba na ndoa za utotoni.

Kauli hiyo imetolewana Mkuu wa Wilaya ya Uyui Gift Msuya wakati akifungua mafunzo ya siku mbili kwa mama wadogo katika Halmashauri ya Wilaya ya Tabora-Uyui yaliandaliwa na Ofisi ya Waziri Mkuu ili kuwajengea uwezo watoto wa kike ambao walikubwa na tatizo la mimba za utotoni.

Alisema lengo la kujenga daharia hizo ni kuwaepusha wanafunzi wa kike wa shule za Sekondari na mimba, vishawishi vinavyowafanya washindwe kuendelea na shule na kuozeshwa na wazazi wao , kuwapa utulivu wa kujisomea kwa kuwa karibu na mazingira ya shule na kuwaepusha kuacha shule kwa sababu ya kutembea umbali mrefu wa kwenda shule ambapo wakati mwingine wanakutana na matatizo ya kutaka kubakwa.

Mkuu huyo wa Wilaya hiyo alisema kuwa kukamilika kwa Daharia hizo sio tu kutasaidia watoto wa Kata husika bali wale wanaotoka Kata jirani ambazo hazina Sekondari ambapo wanafunzi wao wanatembelea umbali mrefu kwenda jirani.
  Afisa Ustawi wa Jamii Mkoa wa Tabora Baraka Makona akitoa maelezo mafupi mafunzo mafupi kwa mama wadogo wa Halmashauri ya Wilaya ya Tabora yaliyojenga kuwajengea uwezo wa kujitambua na kufanya maamuzi sahihi ya kujiwekea 
malengo katika maisha yao.
  Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Vijana kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Julius Toneshi akitoa maelezo mafupi mafunzo mafupi  kwa mama wadogo wa Halmashauri ya Wilaya ya Tabora yaliyojenga kuwajengea uwezo wa kujitambua na kufanya maamuzi sahihi ya kujiwekea malengo katika maisha yao.
 Mkuu wa Wilaya ya Uyui Gift Msuya akifungua  mafunzo mafupi  kwa mama wadogo wa Halmashauri ya Wilaya ya Tabora yaliyolenga kuwajengea uwezo wa kujitambua na kufanya maamuzi sahihi ya kujiwekea malengo katika maisha yao.
 Baadhi ya mama wadogo wakiwa katika mafunzo ya siku mbili mafunzo yalilenga kuwajenga kuwajengea uwezo wa kujitambua na kufanya maamuzi sahihi ya kujiwekea malengo katika maisha yao.
 Mkuu wa Wilaya ya Uyui Gift Msuya (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na mama wadogo  mara baada kufungua  mafunzo mafupi  kwa mama wadogo wa Halmashauri ya Wilaya ya Tabora yaliyolenga kuwajengea uwezo wa kujitambua na kufanya maamuzi sahihi ya kujiwekea malengo katika maisha yao.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...