Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Ndugu Jerry Muro amezindua zoezi la utoaji wa vitambulisho Kwa ajili ya wafanyabiashara ndogondogo maarufu kama wamachinga ambao mauzo ghafi Hayazidi Shilingi milioni 4.

Akizindua zoezi hilo la utoaji wa Vitambulisho ambalo limefanyika katika Halmashauri ya Arusha Dc eneo la Ngaramtoni na Halmashauri ya Meru katika eneo la Uwanja wa Ngaresero ambapo limehudhuriwa na mamia ya wafanyabiashara Ndogondogo ambao watanufaika na zoezi hilo ambapo Kwa kuanzia Wilaya itatoa zaidi ya vitambulisho elfu sita Kwa wafanyabiashara ndogondogo Wilayani Arumeru.

Awali Ndugu Muro akitoa taarifa ya utekelezaji wa zoezi la ugawaji wa vitambulisho hivyo , Meneja wa mamlaka ya mapato nchini TRA Wilayani Arumeru Bwana Musa Sudi amesema wataendelea kutoa Elimu kwa wafanyabiashara ili waweze kutambua fursa zilizopo katika kufanya Biashara kupitia vitambulisho vya Magufuli hatua ambayo itawarahisishia ulipaji wa kodi pamoja na kuwasaidia kukua kibiashara.

Wakizungumza Kwa nyakati tofauti wakati wa zoezi la utoaji wa vitambulisho hivyo , wakurugenzi wa Halmashauri za Arusha na Meru Ndugu Emanuel Mkongo pamoja na Dkt . Charles Mahela wamesema Halmashauri zimeweka utaratibu mzuri wa Kuwatambua wafanyabiashara pamoja na kuwaratibu ili waweze kutambuliwa na kuingizwa kwenye Mfumo rasmi ambao utatoa fursa ya wao kuweza kukua na kuepuka migongano ya mara Kwa mara katika kufanya biashara.
 Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Ndugu Jerry Muro amezindua zoezi la utoaji wa vitambulisho Kwa ajili ya wafanyabiashara ndogondogo maarufu kama wamachinga ambao mauzo ghafi Hayazidi Shilingi milioni 4,kama aonekanavyo pichani DC Muro akimkabidhi mmoja wa machinga kitambulisho hicho,aidha zoezi hilo  limefanyika katika Halmashauri ya Arusha Dc, eneo la Ngaramtoni na Halmashauri ya Meru katika eneo la Uwanja wa Ngaresero ambapo limehudhuriwa na mamia ya wafanyabiashara Ndogondogo
Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Ndugu Jerry Muroakimkabidhi mmoja wa machinga kitambulisho kwa ajili ya wafanyabiashara ndogondogo maarufu kama wamachinga ambao mauzo ghafi Hayazidi Shilingi milioni 4,kama aonekanavyo pichani DC Muro 
 Baadhi ya Wafanyabiashara ndogo ndogo wakiwa wamejitokeza kwa wingi wakisubiri kupewa vitambulisho hivyo,ambavyo vimeonekana kuwa umuhimu mkubwa kwao.

  Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Ndugu Jerry Muro pichani katikati akitoa maelekezo kwa baadhi ya Wafanyabiashra ndogo ndogo,mara baada ya kuzindua zoezi hilo la utoaji wa vitambulisho Kwa ajili ya wafanyabiashara ndogondogo maarufu kama wamachinga ambao mauzo ghafi Hayazidi Shilingi milioni 4.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...