Na Rhoda Ezekiel,Kigoma

WANAFUNZI wa Shule ya Msingi Kichacha katika Kijiji cha Kichacha Kata ya Kasanda wilayani Kakonko mkoani Kigoma wameipongeza Serikali kwa kuwajengea madarasa na kuwatoa chini ya mti walikokuwa wakisomea awali.

Pongezi hizo wamezitoa jana baada ya Mkuu wa Wilaya ya Kakonko Kanali Hosea Ndagala kutembelea shule hiyo na kukuta watoto wakiwa katika vyumba vya madarasa tofauti na awali walipokuwa wakisomea katika nyumba ya miti.

Mwanafunzi wa darasa la tano katika shule hiyo Kulwa Anania amesema walikuwa wakipata wakati mgumu pindi mvua zilipokuwa zikinyesha kwani walikuwa hawaendi shule kwa kuwa walikuwa hawana eneo zuri la kusomea na ilikuwa ikisababisha kushuka kwa ufaulu katika masomo.

Amesema wanaipongeza Serikali kwa kutatua changamoto yao waliokuwa nayo na sasa wanaendelea kusoma vizuri katika mazingira mazuri na wanaipongeza serikali kwa jitihada wanazo zifanya.Kwa upande wake Mkuu wa Shule ya Msingi Kichacha Emanuel Siwija amesema kwa mwaka 2017/2018 walipokea jumla ya Sh. milioni 42 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vinne vya madarasa na vyoo matundu manne na ofisi moja, ambapo mpaka sasa ujenzi huo umekamilika na wanafunzi wanatumia vyumba hivyo.

Amesema awali wanafunzi hao walianza kusomea chini ya mti ,na baadae wakajenga kijumba cha miti kwa ajili ya kujihifadhi na 2018 ndipo walipopata madarasa na mpaka sasa upungufu ni mdogo.Ameongeza kwa mwaka jana wao kama shule kwa matokeo ya darasa la nne wameshika nafasi ya pili katika Wilaya na wanaendelea kupambana kuhakikisha wanafunzi wote wanafaulu kwa kuwa nyenzo za kufundishia wanazo na Serikali imetoa madawati kupitia Mkuu wa Wilaya.

Akiwa katika ziara ya kukagua shughuli za maendeleo Mkuu wa Wilaya ya Kakonko Kanali Hosea Ndagala, amesema wao kama Serikali wamejitahidi sana kuhakikisha suala la upungufu wa vyumba vya darasa linapungua na kuhakikisha Wanafunzi wanapata elimu na katika mazingira bora ya kusomea .

Amesema Serikali itaendelea kushirikiana na wananchi kuhakikisha watoto wote wanapata elimu, na kuwaomba wananchi kuendelea kushirikiana na Serikali kuchangia shughuli za maendeleo bila kujali itikadi zao.

Aidha Mkuu huyo alitoa mwito kwa Wananchi wa Wilaya hiyo kuwapuuza Wale wote wanaowashawishi wananchi kuacha kujitolea katika shughuli za maendeleo kwa kuwa maendeleo yote yanaletwa na Wananchi kwa kushirikiana na Serikali.


Shule ya msingi Kichacha ilivyokuwa mwaka 2017

Mkuu wa Wilaya ya Kakonko Kanali Hosea Ndagala akizungumza na Wanafunzi wa Shule ya Msingi Kichacha katika Kijiji cha Kichacha Kata ya Kasanda wilayani Kakonko mkoani Kigoma,Kanali Ndagala ametembeea shule hiyo na kukuta watoto wakiwa katika vyumba vya madarasa tofauti na awali walipokuwa wakisomea katika nyumba ya miti.
Shule ya msingi Kichacha ilivyo sasa 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...