Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt.Hamisi Kigwangalla amekutana na kufanya mazungumzo  na Wakala wa watalii kutoka  Beijing nchini China, Bw.He Liehui ambaye kwa mwaka huu amepanga kuwaleta watalii 10,000 nchini Tanzania na kwa sasa yupo nchini kwa ajili ya kufanya maandalizi ya watalii hao.

Mazungumzo hayo kati yao  yamefanyika katika ofisi ndogo ya Wizara hiyo Mpingo House jijini Dar es Salaam

Aidha,  Wakala huyo Bw.He  anatarajia pia leo  kuonana na Waziri Mkuu wa Tanzania, Mhe.Kassim Majaliwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...