*Wabunge waanza kuuchambua,Halima Mdee ataka Bunge kuchukua tahadhari


Na Said Mwishehe,Globu ya jamii


WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge,Kazi ,Vijana na Ajira amewasilisha rasmi Bungeni Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Vyama vya Siasa ambapo baada ya kuwasilisha wabunge mbalimbali wameuchambua na kutoa maoni yao.

Hata hivyo baadhi ya wabunge hasa wa Vyama vya Upinzani ambao wamechangia mjadala kuhusu muswada huo wametilia shaka baadhi ua vipengele na kuomba Bunge kuviangalia kwa umakini mkubwa.

Wakati anawasilisha Muswada huo wa Marekebisho ya Sheria vya Vyama vya Siasa Waziri Mhaga ameliambia Bunge leo mjini Dodoma na lengo la muswada huo ni kuwa na sheria ya vyama vya siasa ambayo itamuwezesha Msajili wa Vyama vya Siasa kutekeleza majukumu yake vuzuri.

Amefafanua baadhi ya vipengele vilivyopo kwenye muswada huo ambapo kabla ya hapo aliweka wazi mchakato wa muswada huo ulianza rasmi mwaka 2013 na ilipofika mwaka 2014 ulisimama kupisha mchakato wa Katiba Mpya na mwaka 2015 mchakato ukasimamishwa kupisha uchaguzi Mkuu.

"Muswada wa marebisho ya  Sheria ya Vyama vya Siasa wa mwaka 2018 unalenga kufanya mabadiliko mbalimbali kwa lengo la kumuwezesha Msajili wa Vyama vya siasa kufanya shughuli zake kwa ufanisi." Kama nilivyotangulia kueleza awali mchakato ulianza mwaka 2013 wakati ukusanyaji wa maoni na ilipofika mwaka 2014 ulisimama kwa ajili ya mchakato wa Katiba mpya na mwaka 2015 ulisimama kupisha uchaguzi mkuu.Muswada huu ninaouwasilisha leo hii umegawanyika sehemu kuu mbili,"amesema Waziri Mhagama.

Amefafanua muswada huo unampa nafasi Msajili wa Vyama vya Siasa kutekeleza majukumu yake ambapo akatumia nafasi hiyo kuelezea hatua kwa hatua vipengele vilivyomo kwenye muswada huo kikiwemo kipengele kinachovitaka vyama vya siasa kuheshimu Katiba ya nchi pamoja na alama kuu za Taifa.

Pia kuna vipengele ambavyo vinatoa maelekezo ya vyama vya siasa namna ya kupata viongozi wake pamoja na hatua zinazotakiwa kufuatwa kwa anayetaka kuanzisha chama cha siasa.

 Katika kipengele cha kuanzisha chama cha siasa moja ya sharti ni kwa anayeanzisha kuwa raia wa kuzaliwa wa Tanzania ambacho kinakwenda sambamba na uraia wa wazazi.Kipengele hicho kimeonekana kuibuq mjadala Bungeni.
 
Pamoja na mambo mengine muswada huo kwa mujibu wa Waziri Mhagama amesema  unaweka maelekezo ya jina la chama cha siasa kutofafana na chama kingine ili kuepuka migongano kati ya chama na chama.
Pia amesema muswada unaweka maelekezo ya jina la chama cha siasa kutofafana na chama kingine.Pia muswada huo una kipengele ambacho kinataka vyama vya siasa kuwasilisha orodha ya majina ya viongozi wa ngazi mbalimbali pamoja na kuwepo orodha ya wanachama kwa lengo la kumuwezesha msajili kuwa na kumbukumbu ya vyama husika.

Waziri Mhagama pia amesema muswada huo una kipengele ambacho kinaeleza kuwa  ni marufuku kwa vyama vya siasa kuwa na vikundi vya ulinzi ambapo kipengele hicho nacho kimeibua mjadala kwani wakati Mbunge wa Kawe Halima Mdee(Chadema) wakati anachangia ameonesha kutoridhishwa na uwepo wa kipengele hicho na kuomba Bunge na Kamati ya Katiba na Sheria kuangalia upya kipengele hicho.
Wakati huo huo Mdee wakati anacgangia muswada huo amesema si kweli kwamba wabunge wa vyama vya upinzani pamoja na vyama vya siasa nchini vinaukataa muswada huo kwani mwaka 2009 walipeleka muswada Bungeni kutaka sheria ya vyama vya siasa kufanyiwa marekebisho.

"Kambi ya upinzani bungeni mwaka 2009 tulipeleka muswada bungeni ili kuhakikisha sheria ya vyama siasa inafanyiwa marekebisho lakini ikakataliwa.Hatujawahi kuogopa kukaguliwa jana,leo na kesho,tuache kutumia propaganda katika jambo la Nchi.

"Watu hapa wanasema tusijadili mambo madogo,hivi kujadili jambo linalovunja Katiba ni dogo?Ibara ya 8 C ya muswada huu kinavunja Katiba," amesema Mdee na kufafanua kuna vipengele ambavyo vinaleta ubaguzi na hilo ni huko ni kuvunja Katiba ya nchi.

Amezungumzia pia kipengele ambacho kinataka kuwepo na orodha ya viongozi wa ngazi mbalimbali kwa kupeleka orodha hiyo kwa Msajili sambamba na kuorodhesha majina ya wanachama jambo ambalo ni gumu hasa kwa kuzingatia mwanachama anaweza kujiunga leo na kesho akatoka kwenye chama husika.

Pia ameonesha mashaka na kipengele cha kuzuia vyama vya siasa kuwa na vikundi vya ulinzi ambapo anasema kipengele hicho hakubaliani nacho .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...