Na Zainab Nyamka, 
Globu ya Jamii

KOCHA Mkuu wa timu ya Yanga Zahera Mwinyi amemteua mshambuliaji wa timu hiyo Ibrahim Ajib kuwa nahodha akichukua nafasi ya beki kisiki Kelvin Yondani.
Hatua hiyo imekuja baada ya Yondani kuchelewa kuripoti mazoezini bila kutoa taarifa yoyote  na kuonesha utovu wa nidhamu akiwa kama kiongozi uwanjani.
Zahera amechukua hatua hiyo baada ya Yondani kutoonekana mazoezini licha ya wenzake wote kuanza mazoezi. 
“Haiwezekani unatoa siku tano za mapumziko, mtu hatokei na hakuna taarifa yoyote. Sipendi hii tabia nimemtoa Yondani, nahodha mpya sasa atakuwa ni Ibrahim Ajibu,” alisema.
Ajibu anakuwa nahodha wa Yanga kwa mara ya kwanza baada ya kupendekezwa leo hii na Kocha wa timu hiyo  Zahera akiamua  kumng’oa Yondani kwa madai ya utovu wa nidhamu.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...