Na Khadija Seif, Globu ya Jamii

MWANAMUZIKI wa miondoko ya Bongofleva  Godfrey Tumaini a.k.a ‘Dudu Baya' anashikiliwa na  jeshi la polisi katika kituo cha Oysterbay jijini Dar es Salaam. 

Akizungumza na Michuzi Blog Kamanda wa polisi Kinondoni, Mussa Taibu ameweka wazi kwa sasa Dudubaya anashikiliwa kwa mahojiano.

Hii ni kufatia agizo alilolitoa jana  Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe kwa jeshi la polisi kwa kushirikiana na Baraza la Sanaa (BASATA) kuhakikisha linamchukulia hatua kali Dudu Baya.

Pia Mwakyembe aliweka wazi sababu za kumchukulia hatua mwanamuziki huyo kutokana na makosa ya kumkashifu, aliyekuwa Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji (Clouds Media Group) Marehemu Ruge Mutahaba.

Baada ya amri hiyo, Basata na jeshi la polisi limemfikisha Dudu Baya kituo cha polisi Oysterbay jijini Dar es Salaam. Sanjari na hilo Mwanamuziki huyo anakabiliwa na  Makosa ya matumizi mabaya ya mtandao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...