Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike akitembelea maeneo ya mji wa Serikali Ihumwa, jijini Dodoma yanapojengwa majengo ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi Stadi pamoja na Ofisi ya Waziri Mkuu, Ajira, Vijana na Walemavu, leo januari 31, 2019.
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike akimsikiliza Msimamizi Mkuu wa Kikosi cha Ujenzi cha Magereza katika mradi huo, ACP. Aron Lunyungu alipotembelea katika eneo la ujenzi wa Ofisi Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi Stadi pamoja na Ofisi ya Waziri Mkuu, Ajira, Vijana na Walemavu, leo januari 31, 2019.
Ujenzi wa majengo ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi Stadi pamoja na Ofisi ya Waziri Mkuu, Ajira, Vijana na Walemavu, leo januari 31, 2019 ukiendelea katika hatua mbalimbali kama inavyoonekana katika picha.
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike akisaini kitabu cha ukaguzi katika ujenzi wa Ofisi Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi Stadi pamoja na Ofisi ya Waziri Mkuu, Ajira, Vijana na Walemavu, leo januari 31, 2019(Picha na Jeshi la Magereza). 



…………………….. 

Na ASP. Lucas Mboje, Dodoma 

KAMISHNA Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike leo januari 31, 2019 ametembelea maeneo ya mji wa Serikali Ihumwa, jijini Dodoma yanapojengwa majengo ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi Stadi pamoja na Ofisi ya Waziri Mkuu, Ajira, Vijana na Walemavu ambapo amekiagiza Kikosi cha ujenzi cha Jeshi la Magereza kinachoshiriki katika ujenzi wa ofisi hizo kuzingatia ubora katika ujenzi wa majengo hayo. 

Kamishna Jenerali Kasike amewataka pia Maafisa na askari wanaoshiriki katika ujenzi wa ofisi hizo kuongeza kasi ya ujenzi kama ambavyo Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alivyoagiza lakini wazingatie viwango vya ubora katika ujenzi huo. 

“Hakikisheni ujenzi unafanyika usiku na mchana kama tulivyokwishajipanga lakini zingatieni viwango vya ubora katika ujenzi”. Amesisitiza Jenerali Kasike. 

Aidha, Kamishna Jenerali Kasike amemtaka Msimamizi Mkuu wa Kikosi cha Ujenzi cha Magereza katika mradi huo, ACP. Aron Lunyungu pamoja na Mhandisi Mradi, SSP. Alfred Bundala kuhakikisha kuwa wanakusanya mahitaji yote muhimu katika eneo la ujenzi ili kufanikisha kasi ya ujenzi huo. 

Ujenzi wa majengo ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi pamoja na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi Stadi ulitarajiwa kukamilika mapema ifikapo tarehe 31 Januari 2019 lakini kutokana na changamoto mbalimbali zilizokuwa nje ya uwezo wa Kikosi cha ujenzi cha Jeshi la Magereza, ujenzi huo umechelewa kukamilika kwa wakati na hatua za ukamilishaji zinaendelea kwa kasi ya kuridhisha.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...