Leo (jana) Februari 5/2019 ni siku ambayo Chuo kikuu Cha Urafiki cha Watu wa Urusi(Peoples’ Friendship University of Russia) au maarufu kama Chuo Kikuu Cha Patrice Lumumba kimetimiza miaka 59 tangu kuasisiwa kwake.

Kama Raisi wa Umoja wa vijana wa nchi zote za Afrika chuoni hapo niliwakilisha Waafrika wote katika jopo la Kimataifa katika kusheherekea siku hii kubwa kwa kuongozana na Mkuu wa Chuo hicho Vladimir Philipov na maraisi wa Vijana wa nchi za Kiarabu, nchi za Asia na tulipozuru makao Makuu ya Shirika kubwa la Habari la Urusi la RIA NOVOST na RUSSIA TODAY na kumsikiliza Mkuu wa Chuo akifanya mahojiano na waandishi wa habari na kushiriki mkutano wa Kimataifa. 

Pia nilipata nafasi ya kukutana Naibu Waziri wa Elimu wa Gambia na Balozi wa Gambia kwa Urusi walipohudhuria Mkutano huu.Mkutano huu ulihusu vipi Chuo hiki kuendelea kuanzisha zaidi Uhusiano na vyuo vyengine duniani na kutoa kozi na mafunzo mbalimbali kwa mtandao duniani zaidi ya nchi 70 ikiwepo nchi 20 za Afrika chini ya Programu yake ya GLOBAL CLUSTER PROGRAM. 

Nchi za Afrika zaidi zilizopo kaitka programu hii ni kutokea kusini kama Zambia,Namibia,Zimbabwe, Angola, Msumbiji, Botswana, Afrika ya Kusini. Tanzania imetajwa katika kupata msaada wa mafunzo kwa usafiri wa reli chini ya shirika la TAZARA. 

Hakika tunaendelea kuliwakilisha Taifa Kimataifa zaidi.

Ahsante sana!

Mohamed Mansour.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...