Naibu
Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora,
Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akipanda mti katika eneo la ofisi yake
inayojengwa kwenye mji wa Serikali Ihumwa, jijini Dodoma 
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa akitoa maelekezo kwa Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Mick Kiliba wakati wa zoezi la upandaji miti katika eneo la ofisi yake inayojengwa kwenye mji wa Serikali Ihumwa jijini Dodoma.
Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Mick Kiliba akiandaa eneo kwa ajili ya kupanda mti wakati wa zoezi la upandaji miti katika eneo la Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora inayojengwa kwenye mji wa Serikali Ihumwa jijini Dodoma.
…………………………..
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) mapema leo amewaongoza watumishi wa ofisi yake kupanda miti katika Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora inayojengwa kwenye Mji wa Serikali, Ihumwa jijini Dodoma ili kutekeleza kwa vitendo kampeni ya Makamu wa Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassan ya kulifanya jiji la Dodoma kuwa la kijani.
Mhe Dkt. Mwanjelwa (Mb) amesema, watumishi wa Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora kama kioo cha Utumishi wa Umma nchini, wamejitokeza kuunga mkono kwa vitendo kampeni hiyo ya kulifanya jiji la Dodoma kuwa kijani kwa kupanda miti ili kuwa mfano bora kwa taasisi nyingine za umma ambazo hazijatekeleza kampeni hiyo.
Akiongoza zoezi hilo, Mhe Dkt. Mwanjelwa (Mb) amesema, pamoja na kuunga mkono kampeni ya kulifanya jiji la Dodoma kuwa kijani, Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora inatambua kuwa mazingira ni uhai ndio maana Jumamosi hii, yeye pamoja na watumishi wa ofisi yake wamejitokeza kwa wingi kupanda miti.
Mhe. Dkt. Mwanjelwa (Mb) amewataka watumishi wa ofisi yake kuendelea na moyo wa kujituma katika utekelezaji wa kampeni ya kulifanya jiji la Dodoma ambalo ni Makao Makuu ya Nchi kuwa la kijani.
Aidha, Mhe. Dkt. Mwanjelwa (Mb) amewataka watumishi hao kuhakikisha wanahudumia miti hiyo ili iweze kustawi na kulifikia lengo la kuwa na Dodoma ya kijani.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa akitoa maelekezo kwa Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Mick Kiliba wakati wa zoezi la upandaji miti katika eneo la ofisi yake inayojengwa kwenye mji wa Serikali Ihumwa jijini Dodoma.
Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Mick Kiliba akiandaa eneo kwa ajili ya kupanda mti wakati wa zoezi la upandaji miti katika eneo la Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora inayojengwa kwenye mji wa Serikali Ihumwa jijini Dodoma.
…………………………..
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) mapema leo amewaongoza watumishi wa ofisi yake kupanda miti katika Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora inayojengwa kwenye Mji wa Serikali, Ihumwa jijini Dodoma ili kutekeleza kwa vitendo kampeni ya Makamu wa Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassan ya kulifanya jiji la Dodoma kuwa la kijani.
Mhe Dkt. Mwanjelwa (Mb) amesema, watumishi wa Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora kama kioo cha Utumishi wa Umma nchini, wamejitokeza kuunga mkono kwa vitendo kampeni hiyo ya kulifanya jiji la Dodoma kuwa kijani kwa kupanda miti ili kuwa mfano bora kwa taasisi nyingine za umma ambazo hazijatekeleza kampeni hiyo.
Akiongoza zoezi hilo, Mhe Dkt. Mwanjelwa (Mb) amesema, pamoja na kuunga mkono kampeni ya kulifanya jiji la Dodoma kuwa kijani, Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora inatambua kuwa mazingira ni uhai ndio maana Jumamosi hii, yeye pamoja na watumishi wa ofisi yake wamejitokeza kwa wingi kupanda miti.
Mhe. Dkt. Mwanjelwa (Mb) amewataka watumishi wa ofisi yake kuendelea na moyo wa kujituma katika utekelezaji wa kampeni ya kulifanya jiji la Dodoma ambalo ni Makao Makuu ya Nchi kuwa la kijani.
Aidha, Mhe. Dkt. Mwanjelwa (Mb) amewataka watumishi hao kuhakikisha wanahudumia miti hiyo ili iweze kustawi na kulifikia lengo la kuwa na Dodoma ya kijani.



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...