Na Khadija Seif ,Globu ya jamii

MSANII wa Bongomovie Kulwa Kikumba a.k.a Dude awaonya watanzania wanaobeza uhudi za Serikali ya awamu ya tano.

Dude ameyasema hayo leo Februari 7,2019 wakati wa kutembelea mradi wa reli wa kisasa (SGR) ambapo amesisitiza ni wakati wa kupongeza na kuonesha ushirikiano kwa maendeleo yanayoletwa nchini chini ya Rais Dk. John Magufuli kwani Tanzania kwa sasa ni madhubuti na imara kwa kila sekta hasa ya uchukuzi.

"Hivi karibuni tulishuhudia ndege mbili zikikabidhiwa hiyo ni wazi kuwa Rais Magufuli lengo lake ni kuhakikisha Watanzania hatuko nyuma katika suala la maendeleo,"amesema Dude.

Amesisitiza kuwa ni muhimu kwa wasanii kuwa mabolozi kwa kueleza mambo mambo mazuri yanayofanywa na Serikali na kwamba treni ya kisasa itakapoaza kutoa huduma ya kusafirisha abiria watoe hamasa ili wananchi wengi waitumie treni hiyo katika safari zao mbalimbali.

Wakati huo huo Dude ametumia nafasi hiyo kuwataka wasanii kuwa na umoja ambao utaleta tija kwa maslahi yao pamoja na kuboresha tasnia na kusiwepo kwa matabaka yatakayofanya tasnia kushuka kiwango.
MSANII wa Bongomovie Kulwa Kikumba a.k.a Dude  

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...