Na Chalila Kibuda, Globu ya jamii

FAMILIA ya Ruge Mutahaba imetoa utaratibu wa mazishi ya ndugu yao, ambayo yanatarajiwa kufanyika wiki ijayo mkoani Kagera.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam ,Msemaji wa familia ya Ruge, aliyejitambulisha kwa jina la  Kashasha amesema mipango iliyopangwa na familia ni kuhakikisha wanaufikisha mwili wa Ruge Dar es Salaam siku ya Ijumaa na kuagwa Jumamosi katika ukumbi wa Karimjee.

"Familia imeamua kwamba mwili wa ndugu yetu Ruge utapumzishwa nyumbani mkoani Bukoba siku ya Jumatatu.Siku hiyo ndio tutampumzisha katika nyumba yake ya milele,"amesema.

Ruge Mutahaba  aliyezaliwa mwaka 1970, ni mmoja wa waasisi na Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji wa Clouds Media Group amefariki dunia jana jioni Februari 26 akiwa Afrika Kusini ambako alikuwa anapatiwa matibabu.


ikumbukwe kuwa Ruge ni mmoja wa waanzilishi na waasisi wa Clouds Media.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...