Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi, Meja Jenerali, Jacob Kingu (vazi la kiraia) akisalimiana na Maafisa wa Jeshi la Magereza alipowasili Gereza Kuu Ukonga leo februari 5, 2019 katika ziara yake ya kikazi yenye lengo la ukaguzi wa ujenzi wa makazi ya Maafisa Magereza unaotekelezwa chini ya Wakala wa Majengo Tanzania – TBA katika eneo la Gereza Kuu Ukonga jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi, Meja Jenerali, Jacob Kingu (wa tatu toka kulia) akitoa maagizo kwa Mratibu wa Mradi wa ujenzi wa Makazi ya Maafisa Magereza Ukonga, Mhandisi Khadija Salum(wa tatu toka kushoto) alipotembelea mradi huo leo februari 5, 2019. Kulia ni Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike.
Moja ya majengo ya ghorofa yanayojengwa chini ya Wakala wa Majengo Tanzania – TBA.
Mkuu wa Kiwanda cha Gereza Kuu Ukonga, ACP. John Itambu akimuongoza Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi, Meja Jenerali, Jacob Kingu (vazi la kiraia) sehemu mbalimbali za Kiwanda hicho ikiwemo sehemu ya Useremala pamoja na sehemu ya Ushonaji wa nguo za aina mbalimbali katika Kiwanda hicho(kushoto) ni Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike.
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi, Meja Jenerali, Jacob Kingu (vazi la kiraia) akiangalia baadhi ya samani za Ofisi zinazotengenezwa katika Kiwanda hicho.
Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini, Phaustine Kasike akimwelezea jambo Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi, Meja Jenerali, Jacob Kingu (vazi la kiraia) alipote,mblea Kiwanda cha Useremala cha Gereza Kuu Ukonga.
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi, Meja Jenerali, Jacob Kingu (vazi la kiraia) akiagana na Mkuu wa Gereza Kuu Ukonga, ACP. Widson Mwanangwa baada ya kutembelea Kiwanda cha Magereza, Ukonga leo Februari 5, 2019(Picha na Jeshi la Magereza).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...