Askofu Mkuu wa Dayosisi ya Meru Baba Elias Kitoi Nassari amepongeza kampeni ya Ujenzi wa vyumba vya madarasa inayofanywa na Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Ndugu Jerry Cornel Muro ambapo amesema kanisa mbali na kupongeza linaunga mkono jitihada hizo.

Askofu Nassari amezungumza hayo jana Februari 6/2019 alipomtembelea Mkuu wa wilaya ya Arumeru ofisini kwake kwa lengo la kumpongeza kwa kazi Kubwa anayoifanya katika sekta ya Elimu na Afya huku akiwa ameambatana na Uongozi Mkuu wa kanisa Dayosisi ya Meru akiwepo Mchungaji Ndelekwa Kuvavanael Pallangyo Msaidizi wa Askofu, Ndugu Lazaro Andrew Katibu Mkuu wa Dayosisi na Ndugu Elisate Manyaeli Maturo Mtunza Hazina Wote ni kutoka KKKT Dayosisi ya Meru

Katika kuunga mkono jitihada zinazofanywa na Mkuu wa wilaya ya Arumeru Baba Askofu Nassari amemkabidhi Lori lililoleta shehena ya mifuko ya saruji Kwa ajili ya ujenzi wa madarasa katika halmashauri ya Meru.

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Arumeru Ndugu Jerry Muro mbali na kupokea pongezi na salamu za Kanisa, ameshukuru msaada wa shehena ya mifuko ya saruji iliyotolewa na kanisa, ambapo amemuhakikisha Baba Askofu Nassari kuwa Serikali ya wilaya ya Arumeru itaendelea kushirikiana na kanisa katika sekta zote za utoaji wa huduma Kwa wananchi.
Mkuu wa wilaya ya Arumeru,Mh.Jerry Cornel akimshukuru Askofu Nassari kwa mchango alioutoa katika kuunga mkono kampeni ya Ujenzi wa vyumba vya madarasa aliyekuwa sambamba na Uongozi Mkuu wa kanisa Dayosisi ya Meru akiwepo Mchungaji Ndelekwa Kuvavanael Pallangyo Msaidizi wa Askofu, Ndugu Lazaro Andrew Katibu Mkuu wa Dayosisi na Ndugu Elisate Manyaeli Maturo Mtunza Hazina Wote ni kutoka KKKT Dayosisi ya Meru

Askofu Nassari akimpongeza Mkuu wa wilaya ya Arumeru,Mh.Jerry Cornel Muro ofisini kwake kwa kazi Kubwa anayoifanya katika sekta ya Elimu na Afya huku akiwa ameambatana na Uongozi Mkuu wa kanisa Dayosisi ya Meru akiwepo Mchungaji Ndelekwa Kuvavanael Pallangyo Msaidizi wa Askofu, Ndugu Lazaro Andrew Katibu Mkuu wa Dayosisi na Ndugu Elisate Manyaeli Maturo Mtunza Hazina Wote ni kutoka KKKT Dayosisi ya Meru
Mkuu wa wilaya ya Arumeru,Mh.Jerry Cornel akimshukuru Askofu Nassari kwa mchango alioutoa katika kuunga mkono kampeni ya Ujenzi wa vyumba vya madarasa

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...