Baadhi ya wafanyakazi wa kiwanda cha kubangua korosho cha Korosho Africa Ltd wakiendelea na kazi kiwandani hapo ambapo hadi kufikia jana zaidi ya wananchi 200 wamepata ajira.
Mfanyakazi wa kiwanda cha kubangua Korosho cha Korosho Africa Ltd Tunduru Mkoani Ruvuma Issa Kahesa kulia akimueleza Mkuu wa wilaya ya Tunduru Juma Homera kazi ya ubanguaji wa korosho za Serikali inavyoendelea katika kiwanda hicho.
Mkuu wa wilaya ya Tunduru Juma Homera aliyeinama akiangalia ubora wa korosho za Serikali zinazobanguliwa katika kiwanda cha kubangua korosho cha Korosho Africa Ltd kilichopo Tunduru Mkoani Ruvuma.
Mkuu wa wilaya ya Tunduru Juma Homera akiangalia korosho zilizobanguliwa katika kiwanda cha Korosho Africa Ltd ambacho kimeingia mkataba na Serikali kwa ajili ya kubangua korosho za Serikali zilizonunuliwa katika msimu wa 2018/2019 kutoka kwa wakulima wa wilaya ya Tunduru,kulia ni mfanyakazi wa kiwanda hicho Issa Kahesa. Picha na Amri Mmanja, Ruvuma.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...